Jamii Yaombwa kuwaadhili watoto



JAMII Mkoani Njombe, imeombwa kujitokeza kuwaasili (Kuwa chukua kama ndugu) watoto yatima wanaolelewa katika vituo vya yatima, ambao wazazi wao wamefariki ama watoto hao waliookototwa baada ya kutelekezwa muda mfupi baada ya kuzaliwa ambao  wazazi hawatambuliki.
Wito huo umetolewa na Katika kituo cha yatima ilichopo Hospitali Teule ya Ilembula , inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania KKKT Dayosisi ya Kusini wakati akipokea misaada kutoka Benki ya CRDB Tawi la Makambako.

Kituo hicho chenye watoto 12, kati yake wawili wakiwa hawajulikani wazazi wao baada ya kuokotwa wakiwa wametelekezwa muda mfupi bada ya kuzaliwa, na kuhudumiwa na hospitali hiyo  kupitia mradi shirikishi kati ya serikali na Taasisi binafsi (PPP).
Akipokea msaada huo wenye thamani ya sh. Milioni 1.1, Katibu Utawala wa Hospitali hiyo Bryceson Mbilinyi  alisema, kituo kina changamoto ya walezi  au ndugu kushindwa kuchangia fedha kiasi sh. 2000 tu kila mwezi pamoja na  kuwatelekeza watoto kituoni.
Msaada huo umepokelewa kwa shangwe kituoni hapo, na kwamba utapunguza adha zinazowakabili, lakini pia Wito ukatolewa kwa wadau wengine.
Meneja wa CRDB Tawi la Makambako, Denis Moleka akiongoza timu ya wafanyakazi alisema, ziara ya kutembelea kituo hicho ni sehemu ya wiki la huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka, ambapo Benki hiyo hurudisha fadhira kwa wananchi.

“Benki ya CRDB inampango wake wa kurudisha fadhira kwa wananchi jamii kwa ujumla,asilimia 1 ya faida yake kila mwaka hutumika kwaajili ya kutoa misaada kwa wahitaji hilo ni kwa makao makuu na matawini kwa ujumla”Alisema Moleka.
Upande wao wafanyakazi wa CRDB wakaguswa sana na taarifa ya watoto waliopo kituoni hapo Flora Fuime alisema, ziara hiyo imempa somo kubwa katika maisha yake na kutambua umuhimu wa kujenga tabia ya kuwatembelea mazingira ya wahitaji.
Akizungumzia kuhusu wazazi wanaowatupa watoto baada ya kuzaliwa,Peter  Mwambembe ofisa wa Benki alisema, uzazi wa mpango inahitajika katika jamii ili kuepusha vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga.

“Mimi nadhani suala la yatima haliepukiki lakini kama tutajikita katika  kupanga uzazi vifo vya akina mama vitapungua na kuwa na idadi ndogo ya yatima kama hawa, nawashauri wazazi wenzangu kuzingatia sana uzazi wa mpango”Alisema, Mwambembe.
Bajeti ya kuhudumia watoto hao kwa mwaka mzima haipungui milioni 50, kutokana na changamoto ya ufinyu wa bajeti  wadau wanashauriwa kujitolea kwa hali na mali ili watoto hao waweze kupata huduma stahiki.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment