Kenya haitoi ushirikiano kesi ya Kenyatta

Waendesha mashtaka wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ya ICC wamewaomba majaji wa mahakama hiyo waamue kwamba Kenya haitoi ushirikiano katika kesi ya uhalifu dhidi ya ubinadamu inayomkabili rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta. Mwendesha mashtaka wa ngazi ya juu wa mahakama hiyo Ben Gumpert ameliambia jopo la majaji watatu leo Kenya haitawasilisha vitu wanavyotaka na vilivyoidhinishwa na mahakama hiyo kwamba wanaweza kuviitisha kama ushahidi kutoka kwa nchi hiyo. Iwapo majaji watapitisha uamuzi huo suala hilo litawasilishwa kwa baraza la nchi wanachama, ambalo ni chombo kinachoziwakilisha nchi zilizosaini mkataba wa Roma uliotumiwa kuiunda mahakama ya ICC.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment