Mapigano kati ya India na Pakistan yauwa watu 9

Maafisa wa India wamesema mamia ya watu wameyakimbia makazi yao katika eneo la Kashmir huku wanajeshi wa nchi hiyo wakikabiliana na vikosi vya Pakistan kwenye mapigano makali ambayo mpaka sasa yamewaua watu tisa. Makabiliano ya risasi katika eneo la mpakani ambayo yamekuwa yakishuhudiwa katika siku za hivi karibuni yameibua wasiwasi mkubwa na watu tisa waliuwawa jana pekee, idadi ya vifo inayoelezwa kuwa kubwa kwa siku moja katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja katika eneo hilo. Raia wapatao 10 wa India wamejeruhiwa wakati wanajeshi wa India na Pakistan walipofyetuliana risasi katika eneo linalozozaniwa la Kashmir kwa siku ya pili leo. India na Pakistan zimelaumiana kwa kuchochea ufyetulianaji huo wa risasi ulioanza Jumapili iliyopita.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment