Waasi wa ADF washambulia DRC


Harakati za waasi zimekuwa zikiteteresha uthabiti katika DRC
Jeshi la DRC linasema kuwa watu 26 wameuawa nchini humo katika shambulizi liliofanywa katika mji wa Beni Mashariki mwa nchi.
Shirika moja la kutetea haki za binadamu, linasema kuwa wapiganaji wa kundi la waasi la Uganda la ADF au Allied Democratic Forces , lilivamia mji huo nyakati za usiku.
Wengi, wa waliofariki walikuwa raia wakiwemo watoto.
Kikosi cha Umoja wa Matifa kikishirikiana na wanjeshi wa DRC, kimekuwa kikijaribu kuwatimua waasi hao wa ADF kutoka nchini DRC tangu mwanzoni mwa mwaka huu.
Lakini waasi hao nao pia wamekuwa wakifanya mashambulizi kadhaa katika meizi ya hivi karibuni.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment