Mchezaji tennis namba 1 katika viwango vya ubora Duniani Andy Murray, amefanikiwa kutinga hatua ya Nusu Fainali ya mashindano ya wazi ya tennis ya Barcelona baada ya kumshinda Albert Ramos-Vinolas.Murray amelipa kisasi katika ushindi huo baada ya mchezaji huyo Ramos-Vinolas kumtoa katika hatua ya nne ya mashindano ya Monte Carlo.

Mschezaji huyo kutoka Scotland, amepata ushindi wa seti 2-6 6-4 7-6 (7-4) katika mchezo huo uliodumu kwa takribani masaa mawili na dakika 59. Murray kwa sasa atakabiliwa na Mchezaji Dominic Thiem kutoka nchini Australia kwa mchezo wa hatua ya Nusu Fainali.
Ramos-Vinolas, ambaye anashikilia nafasi ya 19 katika viwango vya ubora vya mchezo huo duniani, alifanikiwa kucheza vizuri zaidi katika seti ya kwanza ya mchezo huo, kabla mambo kugeuka katika seti ya pili ambayo Murray aliweza kufanya vizuri zaidi.

Andy
Murray of Britain reacts during his match against Albert Ramos-Vinolas
of Spain in a quarterfinal match at the Barcelona Open Tennis Tournament
in Barcelona, Spain, Friday, April 28, 2017. (AP Photo/Manu Fernandez)
BY HAMZA FUMO
0 maoni:
Post a Comment