Uber yatumia ''progamu ya kisiri'' kuhepa wakaguzi



Haki miliki ya picha EPA
Image caption Uber imesema inatumia programu hiyo kuwanyima huduma watu wanaoshuku huenda wakabaini mienendo yao
Kampuni ya Magari ya Uber, ya Marekani, imekiri kutumia programu ya kisiri ya kompyuta, kuisaidi kutambua na kuwazuia wakaguzi kupata taarifa,inayotoa ushahidi wowote kwamba inavunja sheria inayoongoza huduma ya usafiri wa texi.
Programu hiyo imeundwa kwa njia ya kipekee, kuwakinga madereva wa kampuni hiyo, dhidi ya watumizi ambao wanaweza kuwawekea mtego kwa lengo la kuwakamata.
Gazeti la The New York Times imefichua kuwa kampuni ya Uber imetumia programu hiyo ya kisiri kuendesha shughuli zake katika miji kama vile Boston na Paris, Hali kadhalika katika mataifa ya Australia, Italia,na China.
Kampuni ya Uber inakabiliwa na tuhuma za ubaguzi kwa misingi ya kijinsia , ushindani mbaya, unaotokana na mtindo wake wa usimamizi na vile vile kuwapunja madereva.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment