Tanzania yampongeza Rais wa Comoro kwa kuimarisha umoja na utulivu


STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
    Zanzibar                                                       16 Septemba, 2014
---
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Moroni, Comoro
Tanzania imempongeza Rais wa Muungano wa Comoro Dk. Ikililou Dhoinine kwa kuimarisha umoja na mshikamo miongoni mwa wananchi wa nchi hiyo ambapo hivi sasa Comoro imekuwa na utulivu na amani.
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema ni jambo la kujivunia kuona wananchi wa visiwa vya Comoro wako katika utulivu, amani na wamekuwa bega kwa bega na Serikali yao chini ya uongozi wa Rais Dhoinine.
 
Akizungumza katika hafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshma yake na mwenyeji wake Rais wa Muungano wa Comoro, Dk. Shein alisema ziara yake nchini humo ina lengo la kuimarisha ushirikiano wa kihistoria na kindugu uliopo baina ya  wananchi wa Tanzania na Comoro.
 
Alimueleza Rais Dhoinine na wageni waliohudhuria hafla hiyo kuwa amefurahishwa na namna Serikali na wananchi wa Comoro wanavyothamini uhusiano wao na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na ushirikiano na ndugu zao wa Zanzibar.
 
“Najisikia niko nyumbani kwa sababu uhusiano wetu umeimarishwa zaidi na mahusiano ya wananchi wake kwa karne nyingi, mahusiano ambayo yamekuwa katika masuala ya kijamii, utamaduni, biashara na mambo mengine mengi” alibainisha Dk. Shein.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment