KOCHA WA UINGEREZA AMESEMA KIKOSI CHAKE NI KIBOVU.



Kocha wa muda wa timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Southgate amesema alirithi kikosi kibovu baada ya kutoka sare ya bila kufungana na Slovenia katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia jana.
Southgate alichukua mikoba ya Sam Allardyce mwezi uliopita kwa ajili ya kuisimamia timu hiyo katika mechi zake nne ambapo mpaka sasa ameshinda mchezo mmoja dhidi ya Malta kabla ya sare ya jana waliyopata.
Uingereza ambao wanaongoza kundi F, walipata alama hiyo moja jana kufuatia juhudi za hali za juu zilizoonyeshwa na kipa wake Joe Hart.
Southgate amesema wakati alipoichukua timu haikuwa sawa lakini taratibu anaona kama kikosi hicho kinaimarika.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment