Sir Elton John akataa kutumbuiza kuapishwa kwa Trump

Sir Elton John akataa kutumbuiza kuapishwa kwa Trump

  • Saa 8 zilizopita
Image caption Mwanamuziki Sir Elton John
Mwanamuziki Sir Elton John hatowatumbuiza wageni katika sherehe ya kuapishwa kwa Donald Trump, msemaji wa msanii huyo maarufu amesema.
Anthony Scaramucci,mmoja wa kikosi cha mageuzi cha bw Trump,aliambia kipindi cha televisheni cha BBC HARDtalk kwamba Sir Elton atawatumbuiza mashabiki mjini Washington DC mwezi Januari.
''Elton ataandaa tamasha wakati wa sherehe za kuapishwa kwa bwTrump'', Scaramucci amesema
Lakini jambo hilo lilipingwa na mwakilishi wa Sir Elton mjini London.
''Hakuna ukweli wowote kuhusu swala hilo,'' aliambia BBC News.
Wakati wa kampeni ,Sir Elton alikuwa akionyesha dalili za kumuunga mkono mpizani wa bw Trump,bi Hillary Clinton wa chama cha Republican.
Akiwatumbuiza mashabiki katika hafla ya uchangishaji wa pesa, ya bi Clinton mjini Los Angeles mwezi Oktoba, aliripotiwa kuuambia umati kwamba: ''Tunahitaji mtu mwenye ubinadamu katika ikulu ya White House,na siyo mtu mjinga''
Bw Trump alikuwa ametumia wimbo wa Sir Elton Rocket Man and Tiny Dance bila idhini ya mwanamuziki huyo katika kampeni zake.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment