Ugonjwa unaoambukiza kama UKIMWI, kati ya watu 100, Nane wanao
 
         
Hospitali
 ya Taifa Muhimbili inatarajia kuanza kufanya uchunguzi wa Virusi vya 
homa ya Ini (Hepatitis B) na kutoa tiba bure kwa wagonjwa 
watakaobainaika kuwa nao kwa kutumia dawa ya Tenefovir katika kipindi 
cha miaka mitano ijayo kuanzia tarehe 1 December 2016.
Tanzania 
itakua nchi ya pili ukanda wa Afrika Mashariki kuanza kutoka huduma ya 
uchunguzi na matatibu ya ugonjwa wa Ini baada ya Rwanda ambayo 
imeshaanza udhibiti wa tiba ya ugonjw ahuo. 
Kwa mujibu
 wa Dr. John Lwegasha ambaye ni Daktari bingwa wa magonjwa ya Ini na 
Matumbo kutoka Hospitali ya Muhimbili amesema nchini Tanzania kati ya 
watu 100 watu nane wameambukizwa Virusi vya homa ya Ini.
0 maoni:
Post a Comment