Video: Wanasheria wakujitolea wa RC Makonda watoa huduma ya kisheria wa wananchi wa chini 10,217

Jopo la wanasheria wa kijitolea wa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda Ijumaa hii wametoa ripoti ya kazi waliyoifanya katika mkoa wa Dar es salaam kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu.
RC Makonda akiwatambulisha wanasheria hao Disemba mwaka jana
Wanasheria hao ambao waligawanywa katika wilaya nne, Kinondoni, Ilala, Kigamboni pamoja na Temeke waliweza kuwafikia wananchi 10,217.
Akiongea na waandishi wa habari mmoja kati ya wanasheria hao wakiwa ofisini kwa mkuu wa mkoa, alisema kwa kipindi hicho kidogo wameweza kusuluhisha migogoro mbalimbali ya wananchi ambayo ilikuwa inatokea kutokana na kukosa msaada wa kisheria.
“Tumeweza kusikiliza kesi za mirathi,ndoa,ajira pamoja na migogoro ya ardhi. Kwa kesi za mirathi tuliwahi kupata malalamiko kutoka kwa msimamizi wa mirathi, amabaye zoezi lake kubwa lilikuwa ni kukusanya mali za marehemu, na alihitajika kuonyeshwa file lenye nyaraka za marehemu kutoka ofisi aliyokuwa akifanyia kazi marehemu, lakini zoezi hilo lilichukua miaka 10, kila mara alikuwa akifuatilia file hilo anaambiwa halipo. Lakini baada ya kufika ofisini kwetu tulifanya mawasiliano na akafanikiwa kuipata file hilo,” alisema Mwanasheria huyo.
Kwa upande wa RC Makonda aliwapongeza wanasheria hao huku akiwataka wanasheria wengine kujitokeza kuwasaidia wananchi ambao wanahitaji msaada wa kisheria.
ANGALIA VIDEO CHIDEO

from Blogger http://ift.tt/2lPU2nT
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment