Mhe.
Lazaro Nyalandu, Waziri wa Maliasili na Utalii akipokewa na Afisa
Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, Suleiman Saleh mara tu alipowasili
katika uwanja wa kimataifa wa Dulles kwa ajili ya kuhudhulia tamasha la
Utalii na miaka 4 ya Blog ya Vijimambo litakalo fanyika Jumamosi Sept
13, 2014. Kushoto ni msaidizi wa Waziri Bwn. Iman Nkuwi.
Msanii
wa kizazi kipya Cassim Mganga akipiga picha na Waziri wa Maliasili na
Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu walipokutana kwenye jengo la Ubalozi wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani ulipo jijini Washington,
DC.
Msanii wa kizazi kipya Cassim Mganga akipata picha za kumbukumbu nje ya mjengo wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
Cassim Mganga akipata picha ya pamoja na Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Bwn. Swele.
Msanii wa Bongo Flava Cassim Mganga akipata picha ya pamoja na wadau wanao tangaza Utalii wa Tanzania nchini Marekani.
Cassim Mganga akisalimiana na Mhe. Liberata Mulamula Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani.
Mwanamuziki
wa kizazi kipya Cassim Mganga akipata picha ya kumbukumbu na Mwambata
wa jeshi Ubalozi wa Tanzani nchini Marekani na Canada, Kanali Adolph
Mutta.
Mwanamuziki wa kizazi kipya Cassim Mganga akipata picha ya kumbukumbu na Aunty Mercy Dachi.
0 maoni:
Post a Comment