AIRTEL YAZINDUA DILI KWA WASANII WOTE

KAMPUNI ya simu za mkononi ya airtel imezindua rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya Airtel Trace Music Stars kwa kurekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi huku baadhi ya wasanii chipukizi wakipata nafasi yakuonyesha vipaji vyao katika viwanja vya Coco Beach

Akizungumza katika uzinduzi huo uliopambwa na burudani mbalimbali ikiwemo Yamoto bendi katika viwanja vya Coco beach jijini Dar es salaam meneja uhusiano wa airtel bw. jackson mmbando amesema kila mtanzania anayo nafasi ya kushiriki katika shindano hilo kwa kupiga simu namba 0901002233.

Aidha Mmbando ameongeza kuwa lengo la kuanzisha shindano hilo ni kuinua vipaji vya watanzania wenye kujua kuimba ili wapate nafasi ya kuwa staa wa kimataifa.

Nae balozi wa shindano hilo Ommy Dimpoz amewaomba watanzania kujitokeze kwa wingi katika kushiriki mashindano hayo ambapo mshindi atajinyakulia zawadi kabambe ikiwemo kurekodi na kusambaziwa nyimbo zake chini ya studio kubwa ulimwenguni pamoja na safari ya kwenda nchini marekani kwa ajili ya kupata mafunzo ya kimuziki na nguli wa muziki wa amerika Akon.
Wasanii wa kundi la yamoto band wakiwa na msanii maarufu nchini ambae pia ni balazo wa airtel trace music stars tanzania Ommy Dimpos wakionyesha namba maalum itakayotumika kupiga na kutuma nyimbo kwa wasanii chipukizi kwenye shindano la airtel trace music stars lililozinduliwa rasmi jana.

Balozi wa airtel music stars Tanzania Ommy Dimpos akitangaza rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya airtel trace music star kwa kukerekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi jana Coco beach.
Meneja uhusiano wa airtel Jackson Mmbando akizindua na kutangaza rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya airtel trace music star kwa kukerekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi jana coco beach.
Baadhi ya wasanii waliojitokeza wakijaribu kuimba na kurekodi kwenye namba maalum ya kushiriki mashindano ya airtel trace music stars katika viwanja vya coco beach ambapo airtel ilimezindua rasmi namba ya kushirmaki shindano la airtel trace music stars kwa lengo la kuwasaidia wasanii wanaochipukia nao kufikia malengo yao ya kuwa nyota wa musiki.
Mmoja kati ya wasanii waliojitokeza akijaribu kuimba kwenye namba maalum ya kushiriki mashindano ya Airtel Trace Music Stars katika viwanja vya coco beach huku meneja uhusiano wa airtel Jackson Mmbando akishuhudia. Airtel imezindua mashindano haya ya Airtel Trace Music stars kwa lengo la kuwasaidia wasanii wanaochipukia nao kufikia malengo yao.

Wasanii wa kundi maarufu na linalofanya vizuri toka TMK yamoto band wakionyesha vitu vyao wakati wa hafla maalum ya uzinduzi wa namba maalum itakayotumika kupiga na kurekodi nyimbo na wasanii chipukizi ili kujishidia dili la kurediwa nyimbo zao marekani kupitia shindano maalum la airtel trace music stars katika viwanja vya coco beach jijini dar es salaam.

Mwisho Urejeshaji Fomu Shindano la Mashujaa wa Kesho ni Oktoba 10

Vijana katika biashara ya uuzaji samaki. Vijana katika biashara ya uuzaji samaki.
Na Mwandishi Wetu, Mtwara 

 WAKATI siku ya mwisho ya urejeshaji wa fomu kwa vijana watakao shiriki Shindano la Mashujaa wa Kesho ukiwadia na dirisha la upokeaji fomu hizo kutarajiwa kufungwa hapo kesho majira ya saa nane idadi ya vijana waliorejesha fomu hizo imeendelea kupanda. 

 Akizungumzia zoezi hilo jana mchana, Ofisa Mawasiliano wa Kampuni ya Statoil Tanzania, Erick Mchome aliwataka vijana waliochukua fomu zao kuzirejesha mapema ili kujipatia fursa ya kushiriki katika shindano hilo ambale linaweza kuwakwamua vijana kiuchumi.
Vijana katika biashara ya uuzaji mapambo mbalimbali 
Vijana katika biashara ya uuzaji mapambo mbalimbali.

 Akifafanua zaidi, Erick Mchome alisema dirisha la kupokea fomu za Shindano la Mashujaa wa Kesho linatarajiwa kufungwa rasmi kesho, Oktoba 10, 2014 majira ya saa nane za mchana na kuwataka vijana wachangamke kabla ya muda huo kufungwa. Alisema bado kuna idadi kubwa ya fomu ambazo hazijarejeshwa na vijana waliochukua fomu hizo na kuwataka kufanya hivyo kabla ya muda wa zoezi hilo kufungwa hapo kesho.

 “Vijana waliorejesha fomu mpaka leo (jana) ni takribani vijana 200. Waliochukua fomu tangu siku ya uzinduzi Septemba 3, 2014 ni zaidi ya vijana 1000. Hivyo natoa wito kwa vijana ambao bado hawajarejesha na wanataka kuingia kwenye ushindani huu kurejesha fomu zao kwa wakati,” alisema Mchome.

 Zoezi zima la urejeshaji fomu litafikia tamati siku ya Ijumaa Oktoba 10, 2014 kabla ya saa nane mchana na baadaye kufanyika mchujo wa kupata vijana 40 watakaoingia hatua ya pili kabla ya kutangazwa washindi watano ifikapo mwezi wa 12. Aidha alivitaja vituo vya kurejesha fomu mkoani Mtwara kuwa ni pamoja na Naliendele Agricultural Institute, Tanzania Institute of Accountancy, VETA, Chuo cha Utumishi, Chuo cha Stella Maris Pamojana Pride FM. 
Vijana katika biashara ya uuzaji samaki. 
Vijana katika biashara ya uuzaji samaki.

 Naye Mhadhiri wa Chuo cha Stella Maris ambaye pia ni Mratibu wa shindano hilo kituo cha chuo hicho, Justin Lusasi aliwataka vijana kutokata tamaa katika ushiriki kwani kitendo cha kushiriki pekee katika shindano hilo na kuingia hatua ya pili ni faida kubwa kwao kwa kuwa watapata fursa ya kujifunza jinsi ya kuaanda mipango ya biashara. 

 “Napenda kuwasihi vijana wote warejeshe fomu zao, wala wasikate tamaa kwani kwa kila atakayefanikiwa kuwa miongoni mwa washiriki 40 watakaoingia katika hatua ya pili, atapata faida kubwa...watapata nafasi ya kujifunza masuala ya biashara kama vile namna ya kuandika mipango ya biashara, utekelezaji na usimamizi wa biashara,” alisema Lusasi. Shindano la Mashujaa wa Kesho linaloendeshwa mkoani Mtwara linalenga kuendeleza ujasiriamali kwa vijana mkoani Mtwara linaratibiwa na kampuni ya uchimbaji gesi ya Statoil Tanzania. 

Washindi watano watapatikana ambapo mshindi wa kwanza atajishindia kitita cha dola za Kimarekani 5,000 na dola 1,000 kwa washindi wengine wanne. Washindi wanatarajia kutangazwa Desemba, 2014.
Vijana katika biashara ya ukaangaji na uuzaji samaki. 
Vijana katika biashara ya ukaangaji na uuzaji samaki.

UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC WAMKARIBISHA BALOZI OMBENI SEFUE KWA CHAKULA CHA JIONI

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiwasili kwenye Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC nchini Marekani alikokaribishwa chakula cha jioni wakiwemo viongozi mbalimbali wa Wizara ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania. Mhe. Ombeni Sefue ndiye aliyewezesha ununuzi wa jengo hilo la Ubalozi wakati alipokua Balozi wa Tanzania nchini Marekani mwaka 2007
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akimpokea Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue siku ya Jumatano Oct 8, 2014 siku Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani ulipomkaribisha chakula cha jioni wakiwemo viongozi mbalimbali wa Wizara ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiongea mawili matatu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dr. Servacius Likwelile.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisalimiana na Naibu Gavana Dr. Natu Mwamba.
Mkuu wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mama Lily Munanka akiongea machche na baadae kumkaribisha Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula.
Mhe. Liberata Mulamula akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na kumshukuru kwa kuwezesha upatikanaji wa jengo hilo la Ubalozi.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akimshukuru Balozi Liberata Mulamula na kuelezea ununuzi wa Jengo hilo ulivyofanyika yakiwemo majengo mengine ya Ubalozi Canada na New York huku akisema ni jambo jema kwa Serikali kuangalia uwezekano wa kununua majengo ya Ubalozi na makazi ya maafisa wake badala ya kukodisha kwani kufanya hivyo kunapunguza gharama kwa kiasi kikubwa sana yeye aliliona hilo ndio maana alipendekeza na hatimae kuwezesha ununuzi wa majengo hayo.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akijichukuli chakula.

Serikali yaweka Mkakati kupunguza changamoto ya ajira kwa Vijana

 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Fatma Mwassa akizungumza na wananchi jana wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora.
 Katibu Mkuu wa Wizaraya Habari.Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akisalimia wananchi jana wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Kudra Mwinyimvua akisalimia wananchi jana wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Fatma Mwassa akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maadhimisho ya wiki ya Vijana jana mkoani Tabora.Kushoto ni ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga,Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Bibi. Kudra Mwinyimvua na wa mwisho kulia ni Mwakilishi wa UNFPA Tausi Hassan.

TSN Group yapongeza kuanzishwa kwa mbio fupi katika Rock City Marathon 2014

 Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah (wapili kushoto)akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 13 Mratibu wa Mbio za Rock City Marathon 2014, Bw. Mathew Kasonta (wa kwanza kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mbio hizo zitafanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Wakishuhudia wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
 Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah  (wapili kulia)akifafanua jambo  kwa waandishi wa habari wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni hiyo kudhamini mbio za Rock City Marathon 2014 zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Wakishuhudia kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, Mratibu wa mbio hizo, Bw. Mathew Kasonta (wapili kushoto) na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
 Mratibu wa mbio za Rock City Marathon, Bw. Mathew Kasonta, (wa pili kushoto) akiongea na waandishi muda mfupi kaba ya kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni ya TSN Group kuoitia kinywaji chake cha Chili Willy kama udhamini wa mbio hizo kwa mwaka huu zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.  Farough Baghozah akifuatiwa na Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari, na kushoto ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto). 
======  =======   =========
Ukurasa mpya umefunguliwa katika mbio za Rock City Marathon za mwaka huu ambapo kwa mara ya kwanza tangu mbio hizo zilipoanzishwa miaka mitano iliyopita, mbio fupi sasa zitakuwepo. 
Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 13 kwa waratibu wa mbio hizo kampuni ya Capital Plus International Limited (CPI), Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN Group Bw. Farough Baghozah aliipongeza hatua hiyo, na kusema kuwa kampuni yake inaungana na wadhamini wengine kuunga mkono tukio hilo la kila mwaka sababu ya dhamira yake ya kuibua na kukuza vipaji vya vijana katika riadha na kukuza utalii wa ndani kupitia michezo.
“Tunayofuraha kuidhamini mashindano ya mwaka huu ambayo sasa yatajumuisha na vijana wadogo ambao wana vipaji vya kukimbia mbio fupi fupi. Hii itawapa vijana wengi nafasi ya kuonyesha vipaji vyao, ambavyo vinaweza kuwa ndiyo fani zao hapo mbeleni,” alisema Bw. Baghozah. 
Alisema kuwa kampuni yake imekuwa ikiunga mkono jitihada mbali mbali zinazolenga kukuza sekta ya  michezo na burudani nchini Tanzania, ambayo imekuwa ikitengeneza fursa za ajira miongoni mwa vijana walio wengi nchini.
 
“Hivi karibuni tu, TSN Group iliweza kuwaleta wachezaji wa timu ya Real Madrid ili kucheza na wachezaji wa zamani wa Tanzania wa mpira wa miguu. Hii ililenga katika kuwatia morari wachezaji wetu na vijana kupenda michezo, wakiendelea kuongeza jitihada ili kufanikiwa zaidi katika kile wanachofanya,” alisema.
Naye mratibu wa tukio hilo, Bw. Mathew Kasonta alisema udhamini huo kutoka TSN Group utasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha mbio hizo za Rock City Marathon 2014, ambapo vipaji katika mchezo wa riadha vitagundulika pamoja na kuyafanya mashindano hayo kuwa chanzo kikubwa zaidi ya kutangaza maeneo mbali mbali ya utalii katika kanda ya ziwa.  
 “Baada ya kupata udhamini toka kwa wadhamini wetu, kamati ya maandilizi ilikaa na kukubaliana kuwa mbio za Rock City za mwaka huu zitajumuisha mbio fupi. Hizi zitajumuisha vijana kutoka katika shule za sekondari na wale waliopo shule za msingi madarasa ya juu. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kuona kuwa mashindano ya marathon nyingi nchini, hayana mbio fupi ambazo zina vipaji vingi pia,” alisema Kasonta.   
Alisema mbio hizo fupi zitakuwa ni; kilomita 100, kilomita 400 na kilomita 1500. Mbio hizo zitafanyika baada ya mbio ndefu ya nusu marathoni. Bw. Kasonta alisema fomu za usajili zinapatikana katika ofisi za kampuni ya Capital Plus International Limited (CPI) jengo la ATC ghorofa ya tatu jijini Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza, Ofisi zote za wilaya za Michezo na Utamaduni mkoani Mwanza, Uwanja wa Nyamagana na pia zinapatikana katika mtandao wa  www.therockcitymarathon.blogspot.com.  
“Meya wa jiji la Mwanza, Bw. Stanslaus Mabula alifungua usajili kwa kuwa mshiriki wa kwanza kujisajili katika mbio za Rock City Marathon 2014 ambazo zitaanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 mwezi Oktoba mwaka huu, ambapo ataonyesha uwezo wake katika riadha kwenye mbio za kilometa 5,” alisema. 
Bw. Kasonta aliwataja wadhamini waliyofanyikisha mbio hizo kuwa ni Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), TSN Group kupitia kinywaji chake cha Chilly Willy, pamoja na African Barrick Gold, IPTL, Air Tanzania, New Mwanza Hotel, Nyanza Bottling, Sahara Media Group, Continental decoders, New Africa Hotel, PPF, Tanapa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).

Wednesday, October 8, 2014

KINANA AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOA WA IRINGA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Kilolo Profesa Peter Msola, alipowasili eneo la Kilolo Minadani, na kufanyiwa mapokezi, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya CCM, katika jimbo hilo, wilaya ya Kilolo mkoani Iringa leo, Oktoba 8, 2014. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Seti Mwamoto
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na mwenyeji wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilolo, Seth Mwamoto baada ya kuwasili katika jimbo la Kilolo wilayani humo leo, 
 Vijana waliojiajiri katika kikundi cha Muungano cha ufyatuaji matofali katika jimbo la Kilolo, wilayani Kilolo mkoani Iringa wakiwa kazini alipowatembelea Kinana leo, Oktoba 8, 2014. Zaidi ya vijana 40 wamo katika muungano huo.
 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji, Umoja wa Vijana wa CCM, Taifa, Seki Kasuga (kushoto) akifuatilia matukio Kinana alipotembelea Umoja wa wajasiariamali wa kikundi cha kufyatua matofali kwa teknolojia ya kisasa katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo mkoani Iringa leo 
 Kinana akizungumza na vijana hao kabla ya kushiriki ufyatuaji matofali. Kulia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye anayefuatana na Kinana kwenye ziara hiyo ya mkoa wa Iringa
 Kinana akisisitiza jambo alipozungumza na vijana wa kikundi hicho kabla ya kushiriki ufyatuaji matofali. Kinana alizitaka mamlaka zinazohusika kuwapatia vijana hao eneo lenye maji ya uhakika kwa ajili ya ufyatuaji matofali, baada ya kumweleza kuwa pamoja na kuufurahia mradi huo wa ufyatuaji matofali lakini wanakumbana na changamoto ya kukosa maji kwa kuwa eneo wanalofanyia mradi huo halina maji.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali akiwa na Prof. Peter Msola (kushoto), alipotembelea mradi wa vijana wajasiriamali wa kikundi cha ufyatuaji matufali kwa teknolojia ya kisasa katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo mkoani Iringa, leo

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua alipotembelea mradi wa vijana wajasiriamali wa kikundi cha ufyatuaji matufali kwa teknolojia ya kisasa katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo mkoani Iringa, leo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofal, alipotembelea mradi wa vijana wajasiriamali wa kikundi cha ufyatuaji matufali kwa teknolojia ya kisasa katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo mkoani Iringa, leo
 Katibu Mkuu wa CCM akipanga matofali baada ya kushiriki ufyatuaji wa matoli kwenye mradi huo wa vijana wa Kilolo 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi kwenye Halmashauri ya Kilolo, pamoja naye Mkuu wa wilaya ya Kilolo Gerald Guninita


BAADAYE KINANA ALIENDA KUCHAPA KAZI IHIMBO

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye viwanja vya zahanati ya Kijiji cha Utengule kata ya Ihimbo, kabla ya kukagua ujenzi wa zahanati hiyo, kwenye jimbo la Kilolo, Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa leo
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia wananchi kwenye viwanja vya zahanati hiyo ya Kijiji cha Utengule
 Wananchi wakisoma utekelezaji wa ilani ya CCM ulivyofanywa na Mbunge wa Kilolo Profesa Peter Msolwa, Kinana alipowasili kwenye zahanati hiyo
 Mbunge wa Kilolo Profesa Msola akieleza alivyosimamia utekelezaji wa ilani ya CCM katika jimbo hilo kwenye mkutano huo
 Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Utengule kwa tiketi ya Chadema, Parcras  Mkakatu akisikiliza maelekezo ya Kinana wakati wa mkutano kwenye zahanati ya Kijiji hicho
 Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Utengule (Chadema), Parcras  Mkakatu akijieleza kwa Kinana wakati wa mkutano kwenye zahanati ya Kijiji hicho
 Mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha Utengule (Chadema), Parcras  Mkakatu akijieleza kwa Kinana wakati wa mkutano kwenye zahanati ya Kijiji hicho
 Wazee wa Kihehe wakimpamba Kinana kwa mavazi rasmi ya keshima ya kabila hilo katika kijiji cha  Utengule, baada ya kuhutubia wananchi kwenyeviwanja vya zahanati ya Kijiji hicho
 Kisha wazee hao wakampa mkuki kukamilisha heshima hiyo
 Kinana akishuka jukwaani baada ya kuwashukuru wananchi kwa wazee hao kumpa heshima ya uchifu
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwaaga wananchi wa Kiijiji cha Utengule baada ya kuzungumza nao katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Zahanati ya Kijiji hicho leo,Oktoba 8, 2014. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment