AIRTEL YAZINDUA DILI KWA WASANII WOTE
KAMPUNI ya simu za mkononi ya airtel imezindua rasmi namba
itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya kusaka vipaji ya
muziki ya Airtel Trace Music Stars kwa kurekodi na kutuma nyimbo zao
kwa kutumia simu zao za mkononi huku baadhi ya wasanii chipukizi
wakipata nafasi yakuonyesha vipaji vyao katika viwanja vya Coco Beach
Akizungumza katika uzinduzi huo uliopambwa na burudani mbalimbali
ikiwemo Yamoto bendi katika viwanja vya Coco beach jijini Dar es
salaam meneja uhusiano wa airtel bw. jackson mmbando amesema kila
mtanzania anayo nafasi ya kushiriki katika shindano hilo kwa kupiga
simu namba 0901002233.
Aidha Mmbando ameongeza kuwa lengo la kuanzisha shindano hilo ni
kuinua vipaji vya watanzania wenye kujua kuimba ili wapate nafasi ya
kuwa staa wa kimataifa.
Nae balozi wa shindano hilo Ommy Dimpoz amewaomba watanzania
kujitokeze kwa wingi katika kushiriki mashindano hayo ambapo mshindi
atajinyakulia zawadi kabambe ikiwemo kurekodi na kusambaziwa nyimbo
zake chini ya studio kubwa ulimwenguni pamoja na safari ya kwenda
nchini marekani kwa ajili ya kupata mafunzo ya kimuziki na nguli wa
muziki wa amerika Akon.
Wasanii wa kundi la yamoto band wakiwa na msanii maarufu nchini
ambae pia ni balazo wa airtel trace music stars tanzania Ommy Dimpos
wakionyesha namba maalum itakayotumika kupiga na kutuma nyimbo kwa
wasanii chipukizi kwenye shindano la airtel trace music stars
lililozinduliwa rasmi jana.

Balozi wa airtel music stars Tanzania Ommy Dimpos akitangaza
rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki mashindano ya
kusaka vipaji ya muziki ya airtel trace music star kwa kukerekodi na
kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi jana Coco beach.
Meneja uhusiano wa airtel Jackson Mmbando akizindua na
kutangaza rasmi namba itakayowawezesha watanzania kushiriki
mashindano ya kusaka vipaji ya muziki ya airtel trace music star kwa
kukerekodi na kutuma nyimbo zao kwa kutumia simu zao za mkononi jana
coco beach.
Baadhi ya wasanii waliojitokeza wakijaribu kuimba na kurekodi
kwenye namba maalum ya kushiriki mashindano ya airtel trace music
stars katika viwanja vya coco beach ambapo airtel ilimezindua rasmi
namba ya kushirmaki shindano la airtel trace music stars kwa lengo la
kuwasaidia wasanii wanaochipukia nao kufikia malengo yao ya kuwa nyota
wa musiki.
Mmoja kati ya wasanii waliojitokeza akijaribu kuimba kwenye
namba maalum ya kushiriki mashindano ya Airtel Trace Music Stars
katika viwanja vya coco beach huku meneja uhusiano wa airtel Jackson
Mmbando akishuhudia. Airtel imezindua mashindano haya ya Airtel Trace
Music stars kwa lengo la kuwasaidia wasanii wanaochipukia nao kufikia
malengo yao.

Wasanii wa kundi maarufu na linalofanya vizuri toka TMK yamoto
band wakionyesha vitu vyao wakati wa hafla maalum ya uzinduzi wa namba
maalum itakayotumika kupiga na kurekodi nyimbo na wasanii chipukizi
ili kujishidia dili la kurediwa nyimbo zao marekani kupitia shindano
maalum la airtel trace music stars katika viwanja vya coco beach
jijini dar es salaam.
Mwisho Urejeshaji Fomu Shindano la Mashujaa wa Kesho ni Oktoba 10
Na Mwandishi Wetu, Mtwara
WAKATI
siku ya mwisho ya urejeshaji wa fomu kwa vijana watakao shiriki
Shindano la Mashujaa wa Kesho ukiwadia na dirisha la upokeaji fomu hizo
kutarajiwa kufungwa hapo kesho majira ya saa nane idadi ya vijana
waliorejesha fomu hizo imeendelea kupanda.
Akizungumzia
zoezi hilo jana mchana, Ofisa Mawasiliano wa Kampuni ya Statoil
Tanzania, Erick Mchome aliwataka vijana waliochukua fomu zao kuzirejesha
mapema ili kujipatia fursa ya kushiriki katika shindano hilo ambale
linaweza kuwakwamua vijana kiuchumi.
Vijana katika biashara ya uuzaji mapambo mbalimbali.
Akifafanua
zaidi, Erick Mchome alisema dirisha la kupokea fomu za Shindano la
Mashujaa wa Kesho linatarajiwa kufungwa rasmi kesho, Oktoba 10, 2014
majira ya saa nane za mchana na kuwataka vijana wachangamke kabla ya
muda huo kufungwa.
Alisema bado kuna idadi kubwa ya fomu ambazo hazijarejeshwa na vijana
waliochukua fomu hizo na kuwataka kufanya hivyo kabla ya muda wa zoezi
hilo kufungwa hapo kesho.
“Vijana
waliorejesha fomu mpaka leo (jana) ni takribani vijana 200. Waliochukua
fomu tangu siku ya uzinduzi Septemba 3, 2014 ni zaidi ya vijana 1000.
Hivyo natoa wito kwa vijana ambao bado hawajarejesha na wanataka kuingia
kwenye ushindani huu kurejesha fomu zao kwa wakati,” alisema Mchome.
Zoezi
zima la urejeshaji fomu litafikia tamati siku ya Ijumaa Oktoba 10, 2014
kabla ya saa nane mchana na baadaye kufanyika mchujo wa kupata vijana
40 watakaoingia hatua ya pili kabla ya kutangazwa washindi watano
ifikapo mwezi wa 12.
Aidha alivitaja vituo vya kurejesha fomu mkoani Mtwara kuwa ni pamoja na
Naliendele Agricultural Institute, Tanzania Institute of Accountancy,
VETA, Chuo cha Utumishi, Chuo cha Stella Maris Pamojana Pride FM.
Vijana katika biashara ya uuzaji samaki.
Naye
Mhadhiri wa Chuo cha Stella Maris ambaye pia ni Mratibu wa shindano hilo
kituo cha chuo hicho, Justin Lusasi aliwataka vijana kutokata tamaa
katika ushiriki kwani kitendo cha kushiriki pekee katika shindano hilo
na kuingia hatua ya pili ni faida kubwa kwao kwa kuwa watapata fursa ya
kujifunza jinsi ya kuaanda mipango ya biashara.
“Napenda
kuwasihi vijana wote warejeshe fomu zao, wala wasikate tamaa kwani kwa
kila atakayefanikiwa kuwa miongoni mwa washiriki 40 watakaoingia katika
hatua ya pili, atapata faida kubwa...watapata nafasi ya kujifunza
masuala ya biashara kama vile namna ya kuandika mipango ya biashara,
utekelezaji na usimamizi wa biashara,” alisema Lusasi.
Shindano la Mashujaa wa Kesho linaloendeshwa mkoani Mtwara linalenga
kuendeleza ujasiriamali kwa vijana mkoani Mtwara linaratibiwa na kampuni
ya uchimbaji gesi ya Statoil Tanzania.
Washindi
watano watapatikana ambapo mshindi wa kwanza atajishindia kitita cha
dola za Kimarekani 5,000 na dola 1,000 kwa washindi wengine wanne.
Washindi wanatarajia kutangazwa Desemba, 2014.
Vijana katika biashara ya ukaangaji na uuzaji samaki.
UBALOZI WA TANZANIA WASHINGTON, DC WAMKARIBISHA BALOZI OMBENI SEFUE KWA CHAKULA CHA JIONI
Katibu
Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiwasili kwenye Ubalozi wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Washington, DC nchini Marekani alikokaribishwa
chakula cha jioni wakiwemo viongozi mbalimbali wa Wizara ya Fedha na
Benki Kuu ya Tanzania. Mhe. Ombeni Sefue ndiye aliyewezesha ununuzi wa
jengo hilo la Ubalozi wakati alipokua Balozi wa Tanzania nchini Marekani
mwaka 2007
Balozi
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata
Mulamula akimpokea Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue siku ya
Jumatano Oct 8, 2014 siku Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
ulipomkaribisha chakula cha jioni wakiwemo viongozi mbalimbali wa Wizara
ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiongea mawili matatu na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dr. Servacius Likwelile.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisalimiana na Naibu Gavana Dr. Natu Mwamba.
Mkuu
wa Utawala na Fedha Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini
Marekani Mama Lily Munanka akiongea machche na baadae kumkaribisha
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula.
Mhe.
Liberata Mulamula akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni
Sefue na kumshukuru kwa kuwezesha upatikanaji wa jengo hilo la Ubalozi.
Katibu
Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akimshukuru Balozi Liberata Mulamula
na kuelezea ununuzi wa Jengo hilo ulivyofanyika yakiwemo majengo mengine
ya Ubalozi Canada na New York huku akisema ni jambo jema kwa Serikali
kuangalia uwezekano wa kununua majengo ya Ubalozi na makazi ya maafisa
wake badala ya kukodisha kwani kufanya hivyo kunapunguza gharama kwa
kiasi kikubwa sana yeye aliliona hilo ndio maana alipendekeza na hatimae
kuwezesha ununuzi wa majengo hayo.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akijichukuli chakula.
Serikali yaweka Mkakati kupunguza changamoto ya ajira kwa Vijana
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Fatma Mwassa
akizungumza na wananchi jana wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya
Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa Wizaraya Habari.Vijana, Utamaduni
na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akisalimia wananchi jana wakati wa uzinduzi wa
maadhimisho ya wiki ya Vijana yanayofanyika katika viwanja vya Ali Hassan
Mwinyi Mkoani Tabora.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Kudra Mwinyimvua
akisalimia wananchi jana wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Vijana
yanayofanyika katika viwanja vya Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Fatma Mwassa
akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maadhimisho ya wiki ya Vijana jana
mkoani Tabora.Kushoto ni ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni
na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga,Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Bibi. Kudra
Mwinyimvua na wa mwisho kulia ni Mwakilishi wa UNFPA Tausi Hassan.
TSN Group yapongeza kuanzishwa kwa mbio fupi katika Rock City Marathon 2014
Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group,
Bw. Farough Baghozah (wapili kushoto)akimkabidhi hundi ya shilingi
milioni 13 Mratibu wa Mbio za Rock City Marathon 2014, Bw. Mathew Kasonta (wa
kwanza kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam
jana. Mbio hizo zitafanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe
26 Mwezi huu. Wakishuhudia wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN
Group Bi. Pamela Mandari, na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi.
Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto).
Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw.
Farough Baghozah (wapili kulia)akifafanua jambo kwa waandishi
wa habari wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13
iliyotolewa na kampuni hiyo kudhamini mbio za Rock City Marathon 2014
zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 Mwezi huu.
Wakishuhudia kulia ni Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela Mandari,
Mratibu wa mbio hizo, Bw. Mathew Kasonta (wapili kushoto) na Afisa Uhusiano na
Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya Kibanga (wa kwanza kushoto).
Mratibu wa mbio za Rock City Marathon,
Bw. Mathew Kasonta, (wa pili kushoto) akiongea na waandishi muda mfupi kaba ya
kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 13 iliyotolewa na kampuni ya
TSN Group kuoitia kinywaji chake cha Chili Willy kama udhamini wa mbio hizo kwa
mwaka huu zitakazofanyika mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26
Mwezi huu. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TSN group, Bw. Farough
Baghozah akifuatiwa na Mkurugenzi wa Operesheni wa TSN Group Bi. Pamela
Mandari, na kushoto ni Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa kampuni hiyo Bi. Koiya
Kibanga (wa kwanza kushoto).
====== ======= =========
Ukurasa
mpya umefunguliwa katika mbio za Rock City Marathon za mwaka huu ambapo kwa mara
ya kwanza tangu mbio hizo zilipoanzishwa miaka mitano iliyopita, mbio fupi sasa
zitakuwepo.
Akizungumza
wakati wa hafla ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 13 kwa waratibu wa mbio
hizo kampuni ya Capital Plus International Limited (CPI), Afisa Mtendaji Mkuu
wa TSN Group Bw. Farough Baghozah aliipongeza hatua hiyo, na kusema kuwa
kampuni yake inaungana na wadhamini wengine kuunga mkono tukio hilo la kila
mwaka sababu ya dhamira yake ya kuibua na kukuza vipaji vya vijana katika
riadha na kukuza utalii wa ndani kupitia michezo.
“Tunayofuraha
kuidhamini mashindano ya mwaka huu ambayo sasa yatajumuisha na vijana wadogo
ambao wana vipaji vya kukimbia mbio fupi fupi. Hii itawapa vijana wengi nafasi
ya kuonyesha vipaji vyao, ambavyo vinaweza kuwa ndiyo fani zao hapo mbeleni,”
alisema Bw. Baghozah.
Alisema
kuwa kampuni yake imekuwa ikiunga mkono jitihada mbali mbali zinazolenga kukuza
sekta ya michezo na burudani nchini Tanzania, ambayo imekuwa ikitengeneza
fursa za ajira miongoni mwa vijana walio wengi nchini.
“Hivi
karibuni tu, TSN Group iliweza kuwaleta wachezaji wa timu ya Real Madrid ili
kucheza na wachezaji wa zamani wa Tanzania wa mpira wa miguu. Hii ililenga
katika kuwatia morari wachezaji wetu na vijana kupenda michezo, wakiendelea
kuongeza jitihada ili kufanikiwa zaidi katika kile wanachofanya,” alisema.
Naye
mratibu wa tukio hilo, Bw. Mathew Kasonta alisema udhamini huo kutoka TSN Group
utasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha mbio hizo za Rock City Marathon 2014,
ambapo vipaji katika mchezo wa riadha vitagundulika pamoja na kuyafanya
mashindano hayo kuwa chanzo kikubwa zaidi ya kutangaza maeneo mbali mbali ya
utalii katika kanda ya ziwa.
“Baada
ya kupata udhamini toka kwa wadhamini wetu, kamati ya maandilizi ilikaa na
kukubaliana kuwa mbio za Rock City za mwaka huu zitajumuisha mbio fupi. Hizi
zitajumuisha vijana kutoka katika shule za sekondari na wale waliopo shule za
msingi madarasa ya juu. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kuona kuwa mashindano
ya marathon nyingi nchini, hayana mbio fupi ambazo zina vipaji vingi pia,”
alisema Kasonta.
Alisema
mbio hizo fupi zitakuwa ni; kilomita 100, kilomita 400 na kilomita 1500. Mbio
hizo zitafanyika baada ya mbio ndefu ya nusu marathoni. Bw.
Kasonta alisema fomu za usajili zinapatikana katika ofisi za kampuni ya Capital
Plus International Limited (CPI) jengo la ATC ghorofa ya tatu jijini Dar es
Salaam, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza, Ofisi zote za wilaya za
Michezo na Utamaduni mkoani Mwanza, Uwanja wa Nyamagana na pia zinapatikana
katika mtandao wa www.therockcitymarathon. blogspot.com.
“Meya
wa jiji la Mwanza, Bw. Stanslaus Mabula alifungua usajili kwa kuwa mshiriki wa
kwanza kujisajili katika mbio za Rock City Marathon 2014 ambazo zitaanza katika
uwanja wa CCM Kirumba tarehe 26 mwezi Oktoba mwaka huu, ambapo ataonyesha uwezo
wake katika riadha kwenye mbio za kilometa 5,” alisema.
Bw.
Kasonta aliwataja wadhamini waliyofanyikisha mbio hizo kuwa ni Shirika la Taifa
la Hifadhi ya Jamii (NSSF), TSN Group kupitia kinywaji chake cha Chilly Willy,
pamoja na African Barrick Gold, IPTL, Air Tanzania, New Mwanza Hotel, Nyanza
Bottling, Sahara Media Group, Continental decoders, New Africa Hotel, PPF,
Tanapa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Wednesday, October 8, 2014
KINANA AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOA WA IRINGA
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Kilolo
Profesa Peter Msola, alipowasili eneo la Kilolo Minadani, na kufanyiwa
mapokezi, akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa ilani
ya CCM, katika jimbo hilo, wilaya ya Kilolo mkoani Iringa leo, Oktoba
8, 2014. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Seti Mwamoto
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na mwenyeji wake, Mwenyekiti wa
CCM Wilaya ya Kilolo, Seth Mwamoto baada ya kuwasili katika jimbo la
Kilolo wilayani humo leo,
Vijana
waliojiajiri katika kikundi cha Muungano cha ufyatuaji matofali katika
jimbo la Kilolo, wilayani Kilolo mkoani Iringa wakiwa kazini
alipowatembelea Kinana leo, Oktoba 8, 2014. Zaidi ya vijana 40 wamo
katika muungano huo.
Mjumbe
wa Kamati ya Utekelezaji, Umoja wa Vijana wa CCM, Taifa, Seki Kasuga
(kushoto) akifuatilia matukio Kinana alipotembelea Umoja wa
wajasiariamali wa kikundi cha kufyatua matofali kwa teknolojia ya kisasa
katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo mkoani Iringa leo
Kinana
akizungumza na vijana hao kabla ya kushiriki ufyatuaji matofali. Kulia
ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye anayefuatana na Kinana
kwenye ziara hiyo ya mkoa wa Iringa
Kinana
akisisitiza jambo alipozungumza na vijana wa kikundi hicho kabla ya
kushiriki ufyatuaji matofali. Kinana alizitaka mamlaka zinazohusika
kuwapatia vijana hao eneo lenye maji ya uhakika kwa ajili ya ufyatuaji
matofali, baada ya kumweleza kuwa pamoja na kuufurahia mradi huo wa
ufyatuaji matofali lakini wanakumbana na changamoto ya kukosa maji kwa
kuwa eneo wanalofanyia mradi huo halina maji.
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali akiwa na
Prof. Peter Msola (kushoto), alipotembelea mradi wa vijana wajasiriamali
wa kikundi cha ufyatuaji matufali kwa teknolojia ya kisasa katika jimbo
la Kilolo wilayani Kilolo mkoani Iringa, leo
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua alipotembelea mradi
wa vijana wajasiriamali wa kikundi cha ufyatuaji matufali kwa
teknolojia ya kisasa katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo mkoani
Iringa, leo
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofal,
alipotembelea mradi wa vijana wajasiriamali wa kikundi cha ufyatuaji
matufali kwa teknolojia ya kisasa katika jimbo la Kilolo wilayani Kilolo
mkoani Iringa, leo
Katibu Mkuu wa CCM akipanga matofali baada ya kushiriki ufyatuaji wa matoli kwenye mradi huo wa vijana wa Kilolo
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi kwenye Halmashauri
ya Kilolo, pamoja naye Mkuu wa wilaya ya Kilolo Gerald Guninita
BAADAYE KINANA ALIENDA KUCHAPA KAZI IHIMBO
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye viwanja vya
zahanati ya Kijiji cha Utengule kata ya Ihimbo, kabla ya kukagua ujenzi
wa zahanati hiyo, kwenye jimbo la Kilolo, Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa
leo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia wananchi kwenye viwanja vya zahanati hiyo ya Kijiji cha Utengule
Wananchi
wakisoma utekelezaji wa ilani ya CCM ulivyofanywa na Mbunge wa Kilolo
Profesa Peter Msolwa, Kinana alipowasili kwenye zahanati hiyo
Mbunge wa Kilolo Profesa Msola akieleza alivyosimamia utekelezaji wa ilani ya CCM katika jimbo hilo kwenye mkutano huo
Mwenyekiti
wa serikali ya Kijiji cha Utengule kwa tiketi ya Chadema, Parcras
Mkakatu akisikiliza maelekezo ya Kinana wakati wa mkutano kwenye
zahanati ya Kijiji hicho
Mwenyekiti
wa serikali ya Kijiji cha Utengule (Chadema), Parcras Mkakatu
akijieleza kwa Kinana wakati wa mkutano kwenye zahanati ya Kijiji hicho
Mwenyekiti
wa serikali ya Kijiji cha Utengule (Chadema), Parcras Mkakatu
akijieleza kwa Kinana wakati wa mkutano kwenye zahanati ya Kijiji hicho
Wazee
wa Kihehe wakimpamba Kinana kwa mavazi rasmi ya keshima ya kabila hilo
katika kijiji cha Utengule, baada ya kuhutubia wananchi kwenyeviwanja
vya zahanati ya Kijiji hicho
Kisha wazee hao wakampa mkuki kukamilisha heshima hiyo
Kinana akishuka jukwaani baada ya kuwashukuru wananchi kwa wazee hao kumpa heshima ya uchifu
Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwaaga wananchi wa Kiijiji cha
Utengule baada ya kuzungumza nao katika mkutano wa hadhara uliofanyika
kwenye Zahanati ya Kijiji hicho leo,Oktoba 8, 2014. Picha zote na Bashir
Nkoromo-theNkoromo Blog




.jpg)
.jpg)
.jpg)










+akifuatilia+matukio+ziara+ya+kinana+Kilolo.jpg)











,+Parcras++Mkakatu+akisikiliza+maelekezo+ya+Kinana+wakati+wa+mkutano+kwenye+zahanati+ya+Kijiji+hicho.jpg)
,+Parcras++Mkakatu+akijieleza+kwa+Kinana+wakati+wa+mkutano+kwenye+zahanati+ya+Kijiji+hicho.jpg)
,+Parcras++Mkakatu+akijieleza+kwa+Kinana+wakati+wa+mkutano+kwenye+zahanati+ya+Kijiji+hicho+1.jpg)




0 maoni:
Post a Comment