Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameonya leo mji wa Kobane
mpakani na Syria unakaribia kuanguka mikononi mwa wapiganaji wa
jihadi wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu akisema harakati ya ardhini
inahitajika kuwashinda wanamgambo hao. Akizungumza wakati wa
hotuba yake aliyoitoa katika mji wa mashariki wa Gaziantep, Erdogan
amesema ugaidi hautakoma mpaka kuwepo ushirikiano wa harakati
ya ardhini dhidi ya wapiganaji hao. Wapiganaji wa Kikurdi wakiungwa
mkono na mashambulizi ya kutokea angani ya Marekani
wamepambana vikali leo na wapiganaji wa Dola la Kiislamu kwenye
makabiliano ya barabarani. Shirika la haki za binadamu la Syria
limesema watu takriban 142, zaidi ya nusu wakiwa wapiganaji wa
jihadi wameuwawa katika mji wa Kobane na viunga vyake tangu
katikati ya mwezi uliopita.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 maoni:
Post a Comment