Hague, Uhollanzi - 08/10/2014. Mwanasheria anaye mtete
Uhuru M Kenyatta, ameiomba mahakama kutupilia mbali kesi inayo mkabili
mteja wake, kwani haina ushahidi wakutosha.
Uhuru M Kenyatta ambaye anashitakiwa kwa kuhusika kwa njia moja au
nyingine katika vurugu ambazo zilisababisha mauaji ya watu wasiopungua
1000 na mali nyingi kuharibiwa wakati wa kampeni za uchaguzi wa urais wa
mwaka 2007 nchini Kenya.
Steven Key,
mwanasheria anaye mtete Uhuru M Kenyatta alisema " hii kesi in kesi
ambayo haina ukweli na kila ukweli unapo ulizwa umekuwa hauwekwi mbele
ya makahama."
" Nahivyo naiomba mahakama kuifuta kesi hii, kwani mpaka sasa upande wa
mashitaka hauna cha kuonyesha kama ushahidi,na wamekubali hilo mbele ya
mahakama."
Uhuru M Kenyatta alihudhurua kwenye kesi hiyo kama Uhuru Kenyatta, na
siyo kama rais wa Kenya, baada ya kukabidhi wadhifa wa Urais wa Kenya
kwa makamu wake William Ruto.

0 maoni:
Post a Comment