WATU WATANO MBARONI KWA KUBADILI “EXPIRE DATE” KWENYE MADAWA YA KILIMO

Watu watano wakiwemo raia wawili wa China na Watanzania watatu wamekamatwa mkoani Mtwara kwa kutuhumiwa kubadili tarehe zilizokwisha muda wa matumizi kwenye dawa za kilimo (expire date) ili dawa hizo ziingizwe tena sokoni na kuonekana bado zinafaa kwa matumizi.
Inadaiwa watuhumiwa hawa wamefanikiwa kubadilisha dawa hizo kwenye mabox zaidi ya mia sita ( 600) na kuzifanya zionekane mpya ambapo Kamanda wa Polisi Mtwara amesema Watuhumiwa hao walikamatiwa Nangwanda.
Makachero wa Polisi baada ya kupewa taarifa waliwahi kwenye eneo la tukio na kukuta watu wanne wakikwangua chupa kuondoa nembo iliyoonyesha dawa hiyo ilitengenezwa tarehe 28 February 2013 na muda wake wa matumizi umekwisha tarehe 27 February 2016.

Nembo mpya feki waliyoitengeneza Wachina hawa inasomeka dawa imetengenezwa tarehe 20 February 2016 na inamaliza muda wa matumizi tarehe 19 February 2019.Wachina wamekamatwa Mtwara wakiwa wanakwangua expire date na kuweka nyingine kwenye dawa ambazo muda wake wa matumizi umeshapita.

from Blogger http://ift.tt/2deAqC3
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment