JESHI LA POLISI KITENGO CHA USALAMA BARABARANI MKOA WA MBEYA KIMEWATAKA WAMILIKI WA VYOMBO VYA USAFILI KUAJILI MADEREVA WENYE LESENI.



                                           MBEYA
Jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani mkoa wa mbeya kimewataka wamiliki wa vyombo vya usafiri kuajiri madereva wenye leseni halali ili kupunguza usumbufu wa vyombo hivyo kutokutembea barabarani.

Hayo yamesemwa na kamanda kamishna wa kikosi cha usalama barabarani wa mkoani mbeya BUTUSYO MWAMBELO wakati wa akizungumza na waandishi wa habari waliotaka kujua  kuhusu madereva wasio na leseni wala kibali chochote ili mradi mliki anamtambua.

Butusyo ametaka halmashauri  jiji kushirikiana kwa pamoja ili kuondoa vibanda vilivyopo kando kando mwa stand kutolewa kwani wamekuwa wakiwauzia madereva,makondakta pamoja na wapiga debe vilevi na kusabisha athari ndani ya jamii.

Aidha BUTUSYO amesema kuanzia tarehe disemba mosi mwaka huu watafanya oparesheni kali itakayofanyika kwa wote wasio na leseni na hawaruhu dereva yeyote asiye na leseni kuingiza usafiri wake barabarani.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa mbeya DHAHIRI KIDAVASHARI amesema kuwa haitaruhusiwa mtu yeyote kuendesha chombo cha moto pindi ifikapo tarehe mosi mwaka huu.

  Na kwa upande wao madereva wamekiri kuwa hii ni changamoto kwao

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment