WANANCHI WA KIBATA WAIMBA WILAYA YA KILWA KUIMALISHA BARABARA.



LINDI
Wananchi wa kijiji cha kibata kilichopo katika kata ya kibata wilayani  kilwa mkoani lindi wameomba halmashauri ya wilaya hiyo kuimarisha barabara za vijijini ili kurahisisha shughuli za usafirishaji kwa kipindi chote cha mwaka .,

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wamesema wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali za usafiri wa barabara katika kipindi cha msimu wa mvua za masika kutokana na hali duni ya miundo mbinu ya barabara inayounganisha kijiji hicho katika kipindi cha mvua za masika na maeneo mengine ya wilaya ya kilwa.

Hayo yanajiri kufuatia gari ya mizigo aina ya kia yenye namba za usajiri T.396 ACQ ikiwa imeanguka na kufunga njia huku bidhaa mbalimbali zikiwa zimesambaa huku na huko ikiendeshwa na kaniso kilipo.


Kwa mujibu wa mashuhuda ambao pia wametoa msaada katika ajali hiyo said abdallah na ally mketo wamesema kuwa tatizo kubwa katika maeneo hayo ni miundombinu  mibovu ya barabara hali inayoweza kusababisha ajali zisizo za lazima.



Mbunge wa kilwa kaskazini THE RASTO NGOMBALE  amesema kuwa wanaitumia barabara hiyo kwa kiasi kikubwa  kutoka dare s salaam kwa kusafirisha mahitaji mbalimbali lakini miundo mbinu yake hairidhishi hivyo wameiomba serikali kuangalia namna ya kusaidia


Mkuu wa mkoa wa lindi godfrey dhambi  akiongozana na mkurugenzi wa halmashauri ya kilwa zabron bugingo kaimu mkuu wa wilaya pamoja na mhandisi na baadhi ya wakuu wa idara amesikiliza kero hizo za wananchi ikiwemo barabara.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment