MAJESHI YA SAUDIA YAENDELEA KUFANYA MAUWAJI DHIDI YA RAIA NCHINI YEMEN.

Ndege za kijeshi za Saudia zimeendelea kufanya mashambulio ya anga katika maeneo mbalimbali ya Yemen na kuzidi kusababisha uharibifu mkubwa na mauaji dhidi ya raia wasio na hatia yoyote wakiwemo wanawake na watoto wadogo.


Kanali ya Televisheni ya al-Mayadeen ya Lebanon imetangaza kuwa, ndege za kijeshi za Saudia zimeshambulia kwa mabomu maeneo kadhaa ya magharibi mwa Yemen na kupelekea kwa akali watu watatu kuuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa.

Ripoti zinaeleza kuwa, miji ya Sa'adah na Sana'a ambao ndio mji mkuu wa Yemen ni miongoni mwa maeneo ambayo yameendelea kushambuliwa kwa mabomu na ndege za kijeshi za Saudi Arabia.
Wakati huo huo, wanajeshi 8 vamizi wa Saudia wameangamizwa katika mji wa Taiz baada ya kushambuliwa na vikosi vya kujitolea vya wananchi. 

Athari za mashambulio ya kinyama ya Saudia nchini Yemen
Majeshi ya Saudi Arabia na washirika wake kama Marekani, Israel na nchi kadhaa za Kiarabu, yalianza kushambulia taifa la Yemen mwezi Machi mwaka jana kwa kisingizio cha kumrejesha madarakani rais aliyetoroka nchi na kukimbilia Saudia, Abd Rabbuh Mansur Hadi.  
Mashambulio hayo ya kinyama ya Saudia hadi sasa yameshaua zaidi ya Wayemeni elfu kumi, kujeruhi mamia ya maelfu ya wengine au kuwaacha bila ya makazi mbali na kuteketeza asilimia 80 ya taasisi za miundombinu na za utoaji huduma na tiba za nchi hiyo masikini ya Kiarabu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment