MEYA ' MBAGUZI' ANG'ATUKA

Meya 'mbaguzi' ang'atuka

  • Dakika moja iliyopita
Image copyright Getty Images
Image caption Michelle Obama
Meya wa mji wa Clay, Jimbo la West Virginia nchini Marekani amejiuzulu, baada ya kuhusika na taarifa za ubaguzi wa rangi dhidi ya Mke wa Rais Obama Michelle Obama.
Beverly Whaling alionekana kuunga mkono taarifa kwenye mtandao wa Facebook iliyomfananisha bi Obama na ''nyani aliyevalia viatu'',.
Meya huyo aliandika kwamba ujumbe huo ulimfurahisa sana, lakini baadae akakanusha na kusema alimaanisha alifurahia matokeo ya uchaguzi Mkuu.Kumekua na saini 170,000 kumtaka meya huyo kuachia ngazi. Bi Whalling ni meya wa mji wa Clay ulio na wakaazi 491 pekee asili mia 98 wakiwa wazungu.
Image copyright WHITE HOUSE
Image caption Melania Trump na Michelle Obama
Meya alichangia ujumbe uliowekwa na bi Pamela Ramsey Taylor mkaazi wa mji huo aliyesema inaridhisha kuona kwamba ikulu ya Rais sasa itakua na Mke wa Rais anayependeza na kwamba amechoshwa kumuona ''nyani aliyevalia viatu'', akiwa ndani ya ikulu.
Licha ya mji wa Clay kuwa na wakaazi wachache hata hivyo ujumbe huu wa Facebook ulisambaa kote nchini na kuzua ghadhabu ya umma kwa kuwa wa kibaguzi. Bi Taylor ameachishwa wadhifa wake kwenye shirika moja la kijamii mji wa Clay. Meya ameomba radhi na kusema majibu yake siyo ya ubaguzi wa rangi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment