uhakiki wa wanafunzi hewa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza




 


TUME iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela kufanya uhakiki wa wanafunzi hewa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza imebaini kuwepo kwa wanafunzi hewa 7,728.
Wanafunzi hao waliisababishia serikali hasara ya Sh milioni 177. Wamebainika baada ya kufanyika uhakiki wa awamu ya pili.


Akiwasilisha taarifa hiyo jana kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), Mwenyekiti wa Tume hiyo, Waryoba Sanya, alisema tume yake ilitumia muda wa siku 28 kufanya uhakiki wake kwa kutumia hadidu za rejea mbili zilizochunguza na kubaini idadi halisi na isiyo halisi ya walimu na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika halmashauri ya jiji la Mwanza.
Alisema tume yake ilitumia takwimu zilizotumika hadi Desemba mwaka 2015 za kuwaletea wanafunzi fedha za elimu bila malipo, ambapo ilibaini kuwepo wanafunzi 102, 065, ambapo kati yao 75,002 walikuwa wanapokea fedha za elimu bila malipo kutoka serikalini.
Alisema katika kufanya uhakiki huo, tume ilitembelea shule 110 na kubaini wanafunzi 27,063 ndio wanaostahili kupelekewa fedha za elimu bila malipo.
Aidha alisema tume ilibaini kuwa walimu 5,385 ndio waliokuwepo kwenye vituo vyao vya kazi na walimu 32 hawakuwepo kwenye vituo vya kazi kwa sababu mbalimbali na kuongeza kuwa kiasi cha Sh bilioni 1.9 kilikuwa kimetumika kwa ajili ya kulipia mpango wa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari kwa halmashauri ya jiji la Mwanza kuanzia Desemba 2015 hadi Agosti mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa, Mongela alisema aliamua kuunda Tume hiyo ili kuondoa mkanganyiko uliokuwepo kati ya uongozi wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya na Taifa na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba, ambapo CWT ilipinga taarifa ya walimu na watumishi hewa iliyotolewa na uongozi wa jiji hilo.
Katika uhakiki wa awali, Kibamba alibaini kuwepo kwa wanafunzi hewa 13,000 na walimu hewa 13,000.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment