Bunge nchini Kenya labadilisha sheria ya Uchaguzi, upinzani wakimbilia Mahakamani

media


Bunge la Kenya
 
Wabunge wa serikali nchini Kenya, limeifanyia marekebisho sheria ya Uchaguzi, kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2017.
Mabadiliko hayo yataiwezesha Tume ya Uchaguzi kutumia njia ya kawaida kuwatambua wapiga kura na kuwasilisha matokeo ya urais ikiwa mfumo wa teknolojia hautawezekana.
Ni mabadiliko ambayo yamepingwa vikali  na wabunge wa upinzani ambao waliondoka bungeni wakati wa mjadala wa kuirekebisha sheria hiyo baada ya kudai kuwa wabunge wa serikali walikuwa wamejihami kwa silaha hatari na walilenga kuwadhuru.
Aidha, upinzani unadai kuwa serikali ya rais Uhuru Kenyatta imebadilisha sheria hiyo ili kutengeneza mazingira ya kuiba kura, madai ambayo serikali inakanusha.
Wabunge wa serikali wanasema, mabadiliko hayo yataipa  nafasi Tume ya Uchaguzi kutumia mfumo mbadala ikiwa mtandao utasumbua siku ya kupiga kura mwezi Agosti mwaka ujao.

mediaBunge la Kenya
Baada ya marekebisho hayo kupitishwa, Mahakama imesema  haiwezi kuzuia kikao cha bunge kuendelea kwa sababu mabadiliko hayo bado hayajawa sheria.
Upinzani umesema utahakikisha kuwa Uchaguzi wa mwaka ujao haufanyiki baada ya kufanyika kwa mabadiliko hayo na hata kutishia kuwepo kwa maandamano.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment