Mazungumzo kuhusu Burundi kufanyika Arusha juma lijalo


mediaMwezeshaji wa mgogoro wa Burundi Benjamin William Mkapa, rais mstaafu wa Tanzaniarfikiswahili/Ali Bilal
Mwezeshaji wa usuluhishi wa mgogoro wa Burundi, Rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa mwanzoni mwa juma lijalo anatarajiwa kuendesha mkutano kwa ajili ya kutathimini hatua iliyofikiwa katika usuluhishi wa mgogoro huo.
Mkutano huo utafanyika jijini Arusha nchini Tanzania na unalenga kuwakutanisha wanasiasa walioko nje ya nchi hiyo ambao hawakupata fursa kushiriki katika mazungumzo ya amani ya awali.
Katika mkutano huo Mkapa atatoa mwenenendo wa mazungumzo ya amani ya Burundi na kuweka bayana changamoto anazokabiliana nazo pamoja na hatua za kuchukua ili mazungumzo hayo yaendelee.
Burundi ilitumbukia katika mgogoro wa kisiasa wakati rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwania muhula wa tatu kinyume na katiba ya nchi hiyo mwaka 2015
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment