Madee na Lulu wafumwa LIVE kwenye gari




eNewz ya EATV imewafuma LIVE wasanii wa bongo fleva Madee na Lulu Diva wakiwa wawili tu ndani ya gari, ambapo Madee amesema kuwa wamekutana kwa ajili ya shughuli za kimuziki na si vinginevyo.
Madee na Lulu
"Sisi tumekuja kwa mambo yetu ya muziki hivyo watu wasije wakaweka unafiki kwenye kuwavurungia mahusiano kwa kuwa Lulu ana mchumba wake na mimi nina girl frend wangu ambaye anampenda sana Lulu Diva, pia". Amesema madee
Kwa upande msanii wa bongo fleva Lulu Diva amepangua skendo zinazoendelea kuhusu yeye na Madee kuwa kwenye mahisiano, na kusema kuwa yeye msanii huyo ni marafiki wa karibu tangu siku nyingi na huwa akikwama mambo mengi huwa anamtafuta ili amsaidiane.
Hata hivyo Lulu alimalizia kwa kusema hana wasiwasi na Madee kwa kuwa ni  kaka yake kwenye muziki tangu siku nyingi na pale anapopata tatizo lolote huwa anamfuata Madee kwa ushauri. 
Itazame hapa

CHANZO EATV.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment