Muimbaji wa ‘Amarula’ amemtaja msanii wa Bongo atakayesikika kwenye albamu yake





Loading...
Msanii Roberto kutoka Zambia amemtaja msanii wa Bongo Fleva, ambaye atasikika kwenye albamu yake mpya.

Muimbaji huyo ambaye amewahi kufanya vizuri kupitia wimbo wake wa Amarula, amemtaja msanii huyo kuwa ni Vanessa Mdee.
“Kuna nyimbo 12 kwenye albamu yangu mpya, pamoja na nyimbo mbili za ziada, hivyo jumla ni 14. Nimewashirikisha wasanii kama Patoranking (Nigeria), Vanessa Mdee (Tanzania), Dammy Krane (Nigeria), Jay Rox (Zambia), kundi la BrathaHood, General Ozzy, Mandela na Young Rico,” amesema Roberto kupitia kipindi cha Mtaa wa Pili cha Choice FM.
Msanii huyo ameongeza kuwa albamu hiyo itaitwa ‘Super Star’ na itatoka Mei 25 mwaka huu.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment