Bunge larekebisha kanuni kuwaruhusu wajumbe walio nje ya nchi Kupiga kura


Image result for Bunge PixBUNGE Maalum la Katiba limepitisha marekebisho ya Kanuni ili kuliwezesha kufikia hatua ya mwisho ya upigaji kura kuanzia tarehe 29 Septemba hadi tarehe 2 Oktoba mwaka huu.  Hatua hiyo ililenga kumaliza vikao vya Bunge hilo kwa muda uliopangwa kwa mujibu wa Sheria wa tarehe 4 Oktoba mwaka huu.  Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta wakati alipokuwa akitoa maelezo ya utangulizi kuhusu uwasilishwaji wa azimio la kupitisha Marekebisho ya Kanuni za Bunge hilo.  Mhe. Sitta amesema kuwa inakadiriwa kuwa wajumbe wasiopungua 480 wanatarajiwa kupiga kura na kutokana na kanuni zilivyokuwa kabla ya mapendekezo ya mabadiliko hayo ingechukuwa siku nyingi kukamilisha zoezi la upigaji kura kwa kupitia kifungu kwa kifungu.  “Kanuni zilivyo hivi sasa kama hatutafanya mabadiliko itachukua kwa wastani wa dakika kama mbili kwa kila mjumbe kupiga kura kwa kila kifungu ambapo kwa siku tutamia wastani wa dakika 960 kwa ibara moja, tunatarajia ibara zitakuwa 300…ameongeza kwa ibara hizo tungehitaji siku 300 kukamilisha zoezi hilo ambao muda huo utakuwa kinyume na utaratibu uliopangwa tutakuwa tunamaliza ibara moja kwa siku moja”, alisema Sitta.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment