Ebola:Watu kusalia nyumbani S:Leone

Rais wa Sierra Leone amesema kuwa serikali inatafakari kutangaza awamu ya pili ya amri ya kutotoka nje kote nchini ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa hatari wa Ebola.Rais Ernest Bai Koroma, amesema kuwa kwa sasa ameridhika na mafanikio yaliyotokana na kuwazuia watu kutoka nje kwa saa 72 .
Awamu ya kwanza ya amri hiyo ilimalizika Jumapili.
Alisema kuwa maafisa wakuu walizuru zaidi ya nyumba milioni moja na kuwapata watu wengi ambao walikuwa wameathiriwa na ugonjwa huo.
Pia walipata mili ya watu waliokuwa wamefariki kutokana na ugonjwa huo.
Shirika la afya duniani limesema kuwa hadi pale hatua zaidi zitakapochukuliwa kukabiliana na janga la Ebola, visa vya maambukizi huenda vikaongezeka.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment