China yalaumiwa kuendeleza mateso


Makampuni nchini China yameingia katika shutuma kali kua wanatengeza na kusafirisha vifaa vya mateso kwa vikosi vya polisi duniani.
Shirika la kutetea haki za binaadamu Amnesty International limetoa taarifa kuwa makampuni yapatayo mia moja na thelathini nchini humo,kati yao wamekiri kutengeneza vifaa hivyo ikiwemo vibanio vya umeme,viti vya umeme,na pingu za vidole gumba.
Inasemekana vifaa vingi japo hutengenezwa na kusafirishwa,vingi matumizi yake ni katika kuleta maumivu mwilini na mateso.
Shirika hilo la kutetea haki za binadamu lina shaka na nchi zenye ukiukwaji mkubwa wa haki za binaadamu hasa Africa na Kusini Mashariki mwa Asia wao ndio wateja wakuu wa vifaa hivyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment