Makabiliano nchini Iraq
Marekani imetekeleza mashambulizi ya angani dhidi ya wapiganaji wa Islamic State karibu na bwawa la Hadatha magharibi mwa Iraq.
Maafisa wa Marekani wamesema kuwa mashambulizi hayo manne ni ya kuwaunga mkono wanajeshi wa Iraq ambao wanalidhibiti bwawa la hadatha lililopo mto Euphrates.
Waziri wa ulinzi nchini humo Chuck Hagel amekana madai kwamba mashambulizi hayo ni ongezeko la ushirika wa Marekani nchini Iraq,akisema kuwa bwawa la Hadatha ni kiungo muhimu cha Iraq na kwamba maslahi ya Marekani yatatishiwa iwapo bwawa hilo litatekwa.
0 maoni:
Post a Comment