Shule ya Iwawa yafanya hafla ya kujipongeza kushika na fasi ya nne kitaifa matokeo kidato cha sita 2014



WALIMU na wanafunzi wa shule ya sekondari Iwawa, wilayani Makete mkoa wa Njombe wametakiwa kutoridhika matokeo ya kitato cha sita iliyoyapata shule hiyo na kushika nafasi ya nne kitaifa 2014 yaliyotangazwa miezi michache iliyopita.  

Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na mkuu wa wilaya ya Makete, Josephine Matiro, katika hafla ya kuwapongeza walimu wa Iwawa sekondari baada ya shule hiyo kushika nafasi ya nne kitaifa, nafasi ya pili kikanda na nafasi ya 1 kwa mkoa wa Njombe katika matokeo ya kidato cha sita mwaka huu.

Matiro aliwataka walimu hao kuongeza jitihada zao za kufundisha pamoja na kuwapongeza wanafunzi kwa moyo wa kujisomea ambavyo kwa pamoja vimepelekea kuitangaza wilaya ya Makete kielimu na kuwataka kupanda na kushika nafasi za juu katika mitihani inayofuata.

“Mnastahili pongezi lakini nawaombeni ongezeni bidii ili mitihani inayokuja mwakani mpande zaidi ya hapa, muitangaze wilaya yetu, tukishirikina pamoja tunaweza" alisema Matiro

Aidha mkuu huyo wa wilaya aliwataka wananchi kushirikiana katika kuchangia maendeleo ya shule kwani serikali inaunga mkono jitihada zao pale tu inapoona wamechangia.

Alisema kumekuwa na kasumba ya watu wachache kuwakatisha tamaa wananchi wengi wenye moyo wakuchangia miradi ya shule, na kusema wananchi wasikatishwe tamaa na watu wa aina hiyo kwani serikali haiwaachii peke yao, wao wakichangia kwa kiasi fulani serikali nayo humalizia.

Matiro alisisitiza kuwa kwa shule zenye upungufu wa walimu, serikali inalitambua tatizo hilo na ndiyo maana inapanga walimu wapya kila mwaka katika shule hizo na mwishowe upungufu huo utamalizika.


Awali akisoma taarifa ya shule, mkuu wa shule hiyo Antony Ng'wavi, alisema shule yake inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa pamoja na walimu jambo ambalo linachangia kupungua kasi ya ufaulu kwa kiasi kikubwa zaidi, huku akiahidi kuwa mwakani shule yake itafanya vizuri kuliko mwaka huu

Mwisho.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment