Ebola:Hofu kwa watoto Marekani




Watoto watano katika jimbo la Texas nchini Marekani waliokutana na mwanamume anayeugua Ebola nchini humo, wanachunguzwa kwa karibu nyumbani kubaini ikiwa wana dalili zozote za ugonjwa huo.
Kwenye mkutano na wandishi wa habari katika hospitali ya Texas Health Presbyterian mjini Dallas, gavana wa jimbo hilo alisema kuwa wazazi wa watoto hao wana wasiwasi lakini aliwahakikishia kuwa hakuna tisho la maambukizi.

Maafisa wamesema kuwa watoto hao wanachunguzwa kwa karibu na nkwamba kuna wanawachunguza watu wengine 12 au zaidi ambao huenda walikaribiana na mwanamume anayeugua Ebola.
Mgonjwa huyo Thomas Duncan anaaminika kuambukizwa Ebola alipokuwa nchini Liberia.
Raia huyo wa Liberia aliingia nchini Marekani wiki mbili zilizopita kuwatembelea jamaa wake, na ni mtu wa kwanza kugunduliwa na Ebola akiwa nchini Marekani.
Bwana Duncan yuko katika hali mbaya kwa mujibu wa wahudum,u wa afya wanamuhudumia.
Muuguzi alimuuliza bwana Duncan alipotembelea hospitali lini alianza kujihisi mgonjwa na ikiwaaliwahi kuwepo katika eneo lililoathirika na Ebola.
Alimwambia kuwa alikuwa ametembelea Liberia, lakini taarifa aliyokuwa anatoa hakuwa ameitoa kwa kikosi kizima kilichohusika na matibabu yake hospitalini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment