Waandishi
wa habari kutoka nchi mbali mbali wakiangalia viungo bandia vya
binadamu, walipotembelea kituo kikuu kinachotengeneza viungo hivyo
nchini India.
Na: Hassan Hamad-India.
Kiasi
cha wagonjwa 65,000 wenye ulemavu wa aina tofauti wanapatiwa visaidizi
pamoja na matibabu kila mwaka nchini India, hatua ambayo huwawezesha
kuendelea na shughuli zao za kimaisha kama kawaida.
Meneja wa kituo kikuu cha viungo bandia vya binadamu katika mji wa Jaipur jimbo la Rajasthan kaskazini mwa India, Om Prakash Sharma ameeleza hayo mbele ya waandishi wa habari kutoka baadhi ya nchi za Afrika, Asia na Latin America waliofika kituoni hapo hivi karibuni kwa ziara maalum ya kimasomo.
Sharma
amesema kituo hicho kijulikanacho kwa jina la “Bhagwan Mahaveer Viklang
Sahayata Samiti (BMVSS), ndio kituo kikubwa zaidi duniani
kinachojihusisha na utengenezaji na utoaji wa viungo bandia vya binadamu
vikiwemo miguu na mikono.
0 maoni:
Post a Comment