Na Asha Salim, Pemba
WAVUVI katika wilaya ya Micheweni wametakiwa
kuchukua tahadhari kubwa juu ya maambukizi ya ugonjwa wa Ebola hasa wanapokuwa
dago nje ya kisiwa cha Pemba.
Tahadhari hiyo imetolewa na Maofisa wa Idara ya Uvuvi, wakati
wakizungumza na wavuvi pamoja na wanajamii katika kijiji cha Shumba mjini, wilayani
humo.
Walisema miongoni mwa watu wanaotakiwa kuchukua tahadhari juu ya
maambukizi ya Ebola ni wavuvi wanaotoka na kuingia katika visiwa tofauti pamoja
na kuacha tabia ya kuchukua wageni kiholela.
0 maoni:
Post a Comment