Na Khamisuu Abdallah
MTOTO Shafik Shaisu Othman (10)
mkaazi wa Fuoni, amefariki dunia wakati akiogelea katika bwawa la kuogelea
liliopo katika bustani ya wanyama Zanzibar Park, wakati akisherekea sikukuu ya
Eid el Hajj.
Akizungumza na Zanzibar Leo
ofisini kwake Muembemadema, Kamanda wa polisi mkoa wa mjini magharibi, Mkadam
Khamis Mkadam, alisema tukio hilo lilitolea juzi saa 8:30 mchana na kusema kifo
chake kilitokana na kuzidiwa na maji.
Alisema polisi wanaendelea na
upelelezi ili hatua ziweze kuchukuliwa.
0 maoni:
Post a Comment