Mtoto afariki akiogelea Zanzibar Park


Na Khamisuu Abdallah

MTOTO Shafik Shaisu Othman (10) mkaazi wa Fuoni, amefariki dunia wakati akiogelea katika bwawa la kuogelea liliopo katika bustani ya wanyama Zanzibar Park, wakati akisherekea sikukuu ya Eid el Hajj.

Akizungumza na Zanzibar Leo ofisini kwake Muembemadema, Kamanda wa polisi mkoa wa mjini magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alisema tukio hilo lilitolea juzi saa 8:30 mchana na kusema kifo chake kilitokana na kuzidiwa na maji.

Alisema polisi wanaendelea na upelelezi ili hatua ziweze kuchukuliwa.

Hivyo aliwataka wazazi kusimamia watoto wao wanapokwenda katika sherehe mbalimbali hasa za sikukuu na kuwashauri wamiliki wa bustani hiyo kuweka kima maalum cha maji kwa watoto na watu wazima ili kuepusha ajali zisizokuwa za lazima
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment