Rais Magufuli amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwachukulia hatua mara moja wale wote watakaobainika kuuza sare za jeshi nchini.

















  
PICHA NA IKULU


Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais Magufuli alifanya ziara hiyo ya kushtukiza jana jioni.




Ikulu imesema Rais Magufuli amepiga marufuku hiyo kutokana na maelezo kutoka kwa baadhi ya askari wa Jeshi la Magereza kwamba wamekuwa wakinunua sare za jeshi hilo kutoka kwa watu binafsi, kinyume cha taratibu za majeshi nchini.




Rais Magufuli amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwachukulia hatua mara moja wale wote watakaobainika kuuza sare za jeshi nchini.








Aidha, Rais Magufuli ametoa Sh bilioni 10 kwa Jeshi la Magereza kwa ajili ya kujenga nyumba mpya zitakazotumika kwa ajili ya makazi ya askari wa Jeshi la Magereza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam.




Hatua hiyo, kwa mujibu wa Ikulu, inatokana na kilio cha askari Magereza kuwa wengi wao wamekuwa wakiishi uraiani, kitu ambacho ni tofauti na taratibu za majeshi nchini na hata kuzorotesha utendaji kazi wa askari wa jeshi hilo.




Rais Magufuli ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu pia ameagiza Jeshi la Magereza kuhakikisha wafungwa wanatumika katika uzalishaji mali badala ya mfumo wa sasa ambao baadhi ya wafungwa wamekuwa wakitumia rasilimali za serikali bila kuzifanyia kazi.




Amewahakikishia maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kuwa serikali itaendelea kuboresha maslahi yao na vitendea kazi kama inavyofanya kwa majeshi mengine nchini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment