UN na EU zalaani shambulizi la kigaidi katika soko nchini Somalia

Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya zimelaani shambulizi la kigaidi lililotokea katika soko la mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.

Taarifa iliyotolewa na Michael Keating, mwakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia imelaani vikali shambulizi lililolilenga soko la mji Mogadishu na imewataka askari wa serikali kuwabaini wahusika wa hujuma hiyo na kuwafikisha mahakamani.

Umoja wa Ulaya pia imelaani hujuma hiyo iliyoua raia kadhaa mjini Mogadishu na  kutangaza azma yake ya kufanya juhudi kubwa kwa ajili ya kudhamini usalama wa taifa hilo la Pembe ya Afrika.
Sehemu ya hujuma za magaidi Somalia
Mripuko wa bomu la kutegwa ndani ya gari uliotokea Jumamosi iliyopita katika lango la kuingilia soko la mji mkuu wa Somalia, Mogadishu uliua zaidi ya raia 10 wengi wao wakiwa wanawake. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na hujuma hiyo, ingawa kundi la kigaidi na kitakfiri la ash-Shabab limehusishwa na jinai hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment