Mimi sipendi kufanya kolabo – Christian Bella


 

Mkali wa masauti Christian Bella amefunguka kwa kusema kuwa hapendi kufanya sana kolabo kwani zinamfanya azoeleke zaidi na mashabiki wake.
christian-bella
Muimbaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa sasa hivi atakuwa anafanya kolabo chache ambazo zitakuwa na faida kubwa katika muziki wake.

“Mimi sipendi sana kufanya fanya kolabo kwa sababu lazima nimlinde Christian Bella,” alisema Bella. “Siwezi kuwa kila muda naimba, huku naimba kule naimba. Lakini mtu akitokea tunafanya na nikiangalia kweli hapa pana umuhimu wa kukaa mimi,”

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na video ya wimbo wake ‘Nishike’ wiki hii amezindua studio yake mpya iitwayo Kingdom Music.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment