WANANCHI WA LUGENGE WATEMBELEA CHANZO CHA MAJI

SIKU chache baada ya wananchi kuomba mradi wa maji ukamilike haraka wamemuomba Rais Kutimiza ahadi yake aliyo itoa akiwa katika viwanja vya Sabasaba Mkoani Njombe na kuamua kufika mpaka katika chanzo cha maji ili kuona maendeleo ya mradi huo.
Wananchi baada ya kufika katika chanzo cha maji wanabaini kuwa mradi huo bado kukamilika kwa kuwa mabomba kutoka katika chanzo hicho bado huku chanzo kingine kikiwa na mashaka kutokana na kilipo na maji yanayopatikana katika chanzo hicho yakiwa ni machache wanawasiwasi wa kuwapo kwa ubadhilifu.
 TAZAMA VIDEO HAPA CHINI








http://ift.tt/1L04AT0
Wakiwa katika chanzo cha pili cha maji wananchi wanashangaa kuona chanzo kilomo na mabomba yanao elekea kuona kuwa kuna mlima ambako maji yanatakiwa kupita na kuwa na wasiwasi wa maji kutoka katika chanzo hicho cha pili na kutokana na maji yanayo zalishwa katika chanzo hicho.

Kinacho wasukuma wananchi hao kufika mpaka katika chanzo cha maji ni kutokana majibu waliyo pata kutoka kwa mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe ambaye aliwaambia bado kilometa saba maeneo ya kutoka kijijini hapo ambapo kuna mabomba ya maji.
Mmoja wa wazee walio fika katika chanzo hicho kilichopo kilimota zaidi ya 20 kutoka kijijini pao Festus Mdoche, anasema kuwa kwakweli kazi bado ni kubwa kwa kuwa katika chanzo mabomba bado hayajafukiwa na kijijini bado kusemekana bado kilometa saba anawasiwasi.
Alisema kuwa pamoja na kuwa kazi bado sana lakini mabomba yal;iyoko maeneo ya chanzo yamepigwa na jua kiasi kwamba yanaweza kuvunjika haya yakigongwa na jiwe kwa kuwa yamekaa muda mrefu juani.
“Kwa kweli kusema bado kilometa saba mimi siamini kwa kuwa huku kwenye chanzo mabomba hayajafukiwa na kwa pale kijijini bado napo hapajafukiwa tunawasiwasi kuwa mradi huu utakamilika mapema,” alisema Mdoche.
Aidha wananchi hawa wanasema kuwa maji wanayotumia kwa sasa ni maji hatari kwa afya yao kwa kuwa wanashiriki pamoja na Mifugo yao.
Akiwa kijijini hapo Matha Malechela, mkazi wa Lugenge anasema kuwa sasa wapo hatarini kupatwa na magonjwa kwa kuwa pamoja na kufuata maji umbari mrefu pia wamekuwa wakitumia maji pamoja na mifugo yao ambapo mifugo hunywa kwa juu huku wao wakichoto kwa chini.
Wanaomba rais Kukumbuka ahadi aliyo waahidi katika mkutano wa hadhara wakati za kampeni oktoba 2015 ambapo rais alimwita mbunge wa jimbo la Njombe na kumuuliza kelo na mbunge alisema kuwa ni maji ya Lugenge ambayo mpaka sasa bado maji hayo.
Mtoto Benito Benadito, anasema kuwa wamekuwa wakitumia muda mwingi kutafuta maji wakitoka na asubuhi kabla ya kwenda shule kwa ajili ya kufanya usafi wao na madarasa wakiwa shuleni hivyo anamuomba rais kuwasaidia kusukuma mradi huo wa maji ili yawafikie.
Hata hivyo Mwenye halmashauri anasema kuwa tatizo ni mkandarasi kutokuwa na fedha na serikali inalipa baada ya kukamilisha kazi.
Anasema wananchi wavumilie kwa kuwa mradi wao huo ni moja ya miradi ya vijiji kumi ambayo inatakiwa kukamilika lakini mradi wao umefikia katika hatua nzuru na kunavijiji ambavyo miradi bado haijaanza.

from Blogger http://ift.tt/2izZkz5
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment