Yanga imeingia mkataba na serikali kuutumia uwanja wa Taifa



Timu ya Dar es Salaam Young Africans leo December 2 2016 imeingia mkataba na serikali kwa ajili ya kupewa kibali cha kutumia uwanja wa Taifa na Uhuru kwa mechi zake za kitaifa na kimataifa.
Kaimu katibu mkuu wa Yanga Baraka Deusdedit amesaini mkataba huo kuiwakilisha Yanga huku upande wa serikali ukiwakilishwa na katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel.
Moja kati ya masharti waliyopewa Yanga katika mkataba huo ili waweze kupata kibali cha kuutumia uwanja huo, kama ikitokea uharibifu wowote utakaofanywa na mashabiki au wachezaji wa Yanga, timu hiyo itaingia gharama za kulipia matengenezo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment