Gospo Kenya: Vipaji vitano vilivyotikisa Kenya 2016 Kwenye Tasnia ya Muziki wa Injili

Mwaka 2016 ni mwaka ulio fana sana kwenye tasnia ya muziki wa Injili Kenya,kwani uliweza kuibuka vipaji vingi na vingine kushika kasi zaidi kwenye nyanja ya muziki wa Injili.

Leo tumekuwekea vipaji vitano ambavyo vilikuwa ni moto wa kuotea mbali ndani ya Kenya,Kama ifuatavyo..
1. DJ Sadic
Sadic anafahamika sana kwa uchezaji santuri (DJ)na pia ni host wa kipindi cha tukuza kinachoruka katika runinga ya KTN kila jumapili. Mchezaji santuri huyu (DJ )alileta  mtazamo mpya alipotoa kibao kipya kwa jina holy ghost party ,wimbo huu wake ulipata umaarufu haswa miongoni mwa vijana nchini Kenya.

2.Producer  Majic Mike
Producer  Majic Mike amekuwa producer  kwa muda sasa lakini kile wengi walikuwa hawamfahamu mpaka pale wimbo wake wa Ayaya ambao aliimba mwenyewe kuingia kwenye tuzo za Groove na wimbo wake wa Light It Up kushinda tuzo za Xtreem.

3. Sammy Dee
kila unapo taja Sammy Dee ,wengi humtambua na kazi ya ubunifu wa video ,kitu ambacho  wengi hawajatambua ni kuwa Sammy Dee alikuwa mmoja wa kundi la Bmf na mwaka huu alirejea kwenye muziki kwa kutoa kibao chake kinachoitwa Overflow
4. Dj Ruff
Baada ya kunyakua  tuzo ya groove kama DJ bora wa mwaka Ruff amezidi kutamba haswa baada ya kuangusha kibao chake na Danny Gift pamoja na J Fam kinachofahamika kama La La La.
5. DJ Tabz
DJ Tabz ni moja  ya Ma DJ maarufu nchini Kenya na  kwa mwaka 2016 alitamba sana baada ya kushirikishwa kama mwimbaji kwenye wimbo wa Give Thanks
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment