MAFUA YA NDEGE YAZUIA MIFUGO RWANDA


Waziri wa kilimo wa Rwanda Geraldine Mukeshimana ametoa wito kwa wafanyabiashara wanaoagiza bidhaa za mifugo kutoka Uganda na nchi za Ulaya kuacha kuagiza kwa muda bidhaa zote za mifugo kutoka Uganda na nchi za Ulaya kutokana na mlipuko wa homa ya mafua ya ndege katika maeneo hayo.
Waziri huyo amewataka wafugaji wote kufungia mifugo yao ili kuepuka mwingiliano kati yao na ndege wasiofugwa, na kwamba watu wanatakiwa kukaa mbali na ndege pori ambao watakutwa wamekufa, na kutoa taarifa haraka kwa mamlaka husika.
Uganda imethibitisha kuwa mlipuko wa ugonjwa huo unaambukiza kwa ndege, ambao pia unaweza kuwapata binadamu. Wizara ya kilimo ya Uganda imesema ndege waliopatwa na ugonjwa huo mpaka sasa ni ndege aina ya Membe, bata na kuku.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment