Kauli ya TFF Kuhusu Watu Wanaotaka kuchoma Kadi za Chama Flani cha siasa Uwanja wa Taifa Leo

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limeonya vikali na kupiga marufuku watu kuingiza siasa katika mchezo wa leo kati ya Simba na Yanga
Akiongea leo na waandishi wa habari,Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema kuwa wamepata taarifa kuna watu fulani leo wanataka kuchana kadi za chama fulani, wengine wanataka kuchoma bendera za chama fulani kupitia mchezo wa leo kati ya Simba na Yanga, hivyo wameonya vikali watu wasijaribu kuingiza siasa zao kwenye michezo na kusema kwa yoyote atakayejaribu yatakayompata asije kuwalaumu TFF

“Kuna watu tumesikia na kuthibitishiwa kwamba kuna watu leo wanataka kuchana kadi za chama fulani cha siasa uwanja wa Taifa mbele ya mashabiki wa Simba na Yanga.


“Kuna wengine wamepanga kuzichoma moto, wako wale wengine wamepanga kuchoma hata bendera za chama hicho, wengine wanasema watafanya ndani ya uwanja wengine nje ya uwanja.


“Nitumie nafasi hii kuwaambia kwamba taarifa tunazo na tunatoa onyo kali kwa yoyote atakaye thubuti kufanya hayo wanayotaka kufanya kwani litakalo mtokea lisijekuwa lawama kwa TFF” alisema Alfred Lucas.

                                        ANGALIA VIDEO CHIDEO

from Blogger http://ift.tt/2kWKwQN
via IFTTT


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment