Kenya Airways kuruka moja kwa moja hadi Marekani




Ndege za Kenya zimepewa kibali cha usalama na maafisa wa Marekani kuanza safari za ndege za moja kwa moja hadi Marekani.
Waziri wa Uchukuzi wa Kenya, James Macharia, alisema kibali hicho kimetokana na kuimarishwa kwa miundombinu katika uwanja mkuu wa ndege mjini Nairobi.
Macharia alisema Kenya inatumai kuwa hatua hiyo itaimarisha biashara kati yake na Marekani na kuongeza mgawo wake wa watalii wa Marekani wanaotembelea nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
Serikali ina hisa katika shirika la ndege la Kenya Airways na hivi karibuni ilimaliza kujenga kituo kipya cha abiria katika uwanja huo na inapanga kutumia fedha zaidi katika kuuboresha Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta. 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment