Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete akiambatana na Waziri Charles Mwijage kukagua eneo ambapo kitajengwa kiwanda cha vigae.
Kikwete
akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast amesema aliweza kujenga
hoja kwa wawekezaji waliokuja nchini kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda
hicho, zilizotosha kuwashawishi ni kwanini wajenge Chalinze badala ya
Mkuranga.
Miongoni mwa hoja alizojenga ni pamoja
na jiografia ya eneo la Chalinze kuwa kitovu cha mikoa karibu yote ya
Tanzania kwa kuwa ni njia panda, na pia Chalinze kuwa ni kitovu cha
kibiashara kwa kuwa kuna urahisi wa usafirishaji wa bidhaa hiyo kwenda
mikoa mbalimbali na hata nje ya nchi.
Pia amesema Chalinze ni eneo ambapo kuna
urahisi wa kupata malighafi kwa ajili ya utengezaji wa bidhaa hiyo,
ambapo Chalinze ni katikati ya maeneo yote ambako malighafi hizo
zinaweza kupatikana ikiwa ni pamoja na Pugu, Rufiji, Iringa na Morogoro.
"Hawa watu wa Tryphod walipokuja, kwanza
walitaka kuwekeza Mkuranga, nikapata fursa ya kwenda kuonana na Meneja
Rasilimali Watu wao, nikazungumza nao, na nikamueleza kuwa fursa kubwa
za kibishara ziko Chalinze". Amesema Kikwete
Amesema baada ya kuwashawishi,
walimuelewa na kukubaliana naye, huku akiungwa mkono pia na Waziri wa
Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.
Ametaja miongoni mwa manufaa
yatakayopatina ni pamoja na fursa ya ajira kati ya 6000 hadi 8000 kwa
wakazi wa eneo hilo na nje ya eneo hilo, na tayari ujenzi umekwishaanza.
0 maoni:
Post a Comment