Kuanzia sasa, kwa mtu yeyote
atakayekutwa na shamba la dawa za kulevya aina ya banngi, anaweza kutiwa
hatiani na kuhukumiwa kifungo cha kuanzia miaka 30 gerezani
Shamba la bangi tayari kwa kuteketezwa, huku mtuhumiwa wa kilimo hicho akiwa chini ya ulinzi (Picha: Maktaba)
Adhabu
hiyo ni kwa mujibu wa Sheria Mpya ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana
na dawa za kulevya, ambayo imeanza kutekelezwa hivi karibuni.
Mbali na adhabu hiyo, sheria hiyo pia
imeweka adhabu ya kifungo cha maisha kwa mtu atakayebainika kusafirisha
aina yoyote ya dawa za kulevya, pamoja na wale wanaoingiza dawa kutoka
nje ya nchi.
Pia sheria hiyo inatoa adhabu ya faini
ya shilingi milioni 200 na kifungo cha maisha kwa watakaokutwa na
malighafi au maabara za kutengezea dawa za kulevya huku ikiweka adhabu
ya kifungo cha miaka mitano na/au faini ya kuanzia shilingi milioni moja
kwa mtu atakayekutwa na kiasi kidogo cha dawa cha dawa za kulevya.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Sheria
na Katiba Dkt. Harrison Mwakyembe, akiwa kwenye kipindi cha East Africa
Breakfast, kwa ajili ya uchambuzi wa sheria hiyo mpya, ambapo pia
ameelezea utofauti wa sheria hiyo ya mwaka 2015 na ile iliyokuwepo ya
mwaka 1995.
Amesema lazima kutakuwa na ukosoaji kwa
kuwa sheria hiyo ni mpya hsa katika suala la mashahidi, lakini kuna
sheria nyingine ya kulinda mashahidi (Whistle Blowers Act), ambayo
itasaidia kuwalinda watu wanaotoa taarifa kuhusu wahusika wa dawa za
kulevya
Amesema pia serikali iko tayari kupokea
maoni kutoka kwa wadau, juu ya nini kifanyike ili kuwadhibiti wahusika
wa dawa za kulevya ambao wamekuwa wakiifanyia wema jamii inayowazunguka
kwa kiasi kikubwa.
Huyu hapa Dkt Mwakyembe akifafanua
0 maoni:
Post a Comment