Ukikutwa na shamba la bangi, jela miaka 30



Kuanzia sasa, kwa mtu yeyote atakayekutwa na shamba la dawa za kulevya aina ya banngi, anaweza kutiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha kuanzia miaka 30 gerezani

 
Shamba la bangi tayari kwa kuteketezwa, huku mtuhumiwa wa kilimo hicho akiwa chini ya ulinzi (Picha: Maktaba)
Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Sheria Mpya ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na dawa za kulevya, ambayo imeanza kutekelezwa hivi karibuni.
Mbali na adhabu hiyo, sheria hiyo pia imeweka adhabu ya kifungo cha maisha kwa mtu atakayebainika kusafirisha aina yoyote ya dawa za kulevya, pamoja na wale wanaoingiza dawa kutoka nje ya nchi.
Pia sheria hiyo inatoa adhabu ya faini ya shilingi milioni 200 na kifungo cha maisha kwa watakaokutwa na malighafi au maabara za kutengezea dawa za kulevya huku ikiweka adhabu ya kifungo cha miaka mitano na/au faini ya kuanzia shilingi milioni moja kwa mtu atakayekutwa na kiasi kidogo cha dawa cha dawa za kulevya.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Sheria na Katiba Dkt. Harrison Mwakyembe, akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast, kwa ajili ya uchambuzi wa sheria hiyo mpya, ambapo pia ameelezea utofauti wa sheria hiyo ya mwaka 2015 na ile iliyokuwepo ya mwaka 1995.

Amesema lazima kutakuwa na ukosoaji kwa kuwa sheria hiyo ni mpya hsa katika suala la mashahidi, lakini kuna sheria nyingine ya kulinda mashahidi (Whistle Blowers Act), ambayo itasaidia kuwalinda watu wanaotoa taarifa kuhusu wahusika wa dawa za kulevya
Amesema pia serikali iko tayari kupokea maoni kutoka kwa wadau, juu ya nini kifanyike ili kuwadhibiti wahusika wa dawa za kulevya ambao wamekuwa wakiifanyia wema jamii inayowazunguka kwa kiasi kikubwa.
Huyu hapa Dkt Mwakyembe akifafanua


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment