Show ya Love, Melodies & Lights iliyofanyika Jumamosi hii katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es salaam ilikuwa ni show ya aina yake katika historia ya burudani ya muziki nchini.
Jux
Show hiyo ilikuwa maalum kwa wasanii watatu, Barakah The Prince, Ben Pol pamoja na Jux huku surprise kibao za wasanii zikitawala usiku huo wa burudani ya aina yake. Wasanii hao waliimba nyimbo zao live pamoja na nyimbo za wasanii wa zamani.
Waziri wa habari, utamaduni sanaa na michezo, Nape Nnauye alihudhuria show hiyo iliyokusanya mastaa mbalimbali wa muziki, filamu pamoja na wabunge.
Pia wasanii wa zamani walitunukiwa vyeti kutokana na mchango wao katika tasnia ya muziki.
Miongoni mwa wasanii waliopandishwa kama surprise ni pamoja Saida Karoli pamoja na watoto wa msanii mkongwe wa muziki Barakah Mushehe. Angalia picha.
Jux akifanya yake
Jux
Jux na Joh Makini
Barakah The Prince
Mashabiki wakiwa na mzuka
0 maoni:
Post a Comment