Simu aliyopokea Nay wa Mitego kutoka BASATA baada ya kutoa wimbo mpya



Rapper kutoka bongoflevani Nay wa Mitego amesema kuwa muda mfupi baada ya kuachia wimbo wake mpya unaoitwa ‘muda wetu‘ amepigiwa simu na Katibu mtendaji wa Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) Mr. Godfrey Mngeleza.
Nay wa Mitego amesema ni tofauti na alivyofikiria kwani baada ya kupokea simu hiyo ya katibu mtendaji wa baraza hilo amemsifia kwa mashairi na maudhui yaliyopo kwenye wimbo wake huo mpya aliouachia rasmi leo Feb 16 kwenye vituo na mtandao.
Nay wa mitego ameyazungumza hayo alipokua kwenye mahojiano na XXL ya CloudsFM na amesema hii kwake ni mara ya kwanza kupigiwa simu na kusifiwa na BASATA >>> ‘Miongoni mwa watu walionipigia simu baada ya kuusikia wimbo huu ni Katibu wa Basata kasema una maudhui mazuri,hii ni mara yangu ya kwanza kusifiwa na Basata’
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment