TRENI ZISIZO NA DEREVA KUTENGENEZWA


Shirika la reli la Uingereza linaloundwa na makampuni mbalimbali ya reli limetoa ripoti ya maendeleo ya reli ikisema katika siku zijazo kampuni hiyo itaboresha miundombinu na vifaa vya reli, na kutumia treni mpya zisizo na dereva, ili kuinua ufanisi na kukidhi mahitaji ya usafiri wa treni yanayoongezeka siku hadi siku.
 
Shirika hilo limetoa mapendekezo mbalimbali ya kuendeleza teknolojia za usafiri wa treni, ikiwemo kutumia treni "zenye akili" ambazo zinawasiliana kupitia sensa na vyombo vya kutoa ishara, ili kujiendesha zenyewe na kuepuka kugongana.
 
Treni zisizo na dereva zikitumiwa kwa wingi, si kama tu usafiri huo utakuwa na ufanisi mkubwa zaidi, bali pia hali ya kuchelewa kwa treni haitatokea mara kwa mara. Aidha, gharama ya nguvu kazi ni ya juu nchini Uingereza, hivyo treni zisizo na dereva zikitumiwa, inakadiriwa kwamba kwa ujumla makampuni ya reli ya Uingereza yatapunguza gharama ya nguvu kazi kwa pauni milioni 340 kila mwaka.
 
Ripoti hiyo pia inasema serikali ya Uingereza imetunga mpango wa uwekezaji wenye thamani ya pauni milioni 45 ili kuendeleza reli zinazotumia teknolojia mpya. Teknolojia ya upashanaji ishara itafanyiwa majaribio, ambayo ni hatua ya kwanza ya kuendeleza treni zisizo na dereva.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment