Wapata mlo na kisha kutimka mbio kutoka hotelini bila kulipa



Haki miliki ya picha Google
Image caption Watu hao walitimka mbio kutoka mgahawa wa El Carmen
Takriban watu 120 waliokuwa wakipata maankuli kwenye mgahawa mmoja kaskazini magharibi mwa Uhispania, walikimbia wote kwa pamoja na kukosa kulipa.
Watu hao raia wa Romania ambao walikuwa mwanzo wamelipa euro 900, waliondoa kwenye mgahawa wa El Carmen wati walikaribia kupata mlo wa keki.
"Ilitokea kwa dakia moja tu, ni kitu walikuwa wamepanga kwa sababu walitoka kwa kutimka mbio." alisema mmiliki wa hoteli Antonio Rodriguez .
Sasa wana deni la euro 2,000 kwenye hoteli hiyo.
Watu hao walikuwa wamepata chakula cha kwanza, chakula kikuu, na chupa 30 za mvinyo, na Rodriguez anasema kuwa hiyo ndiyo mara ya kwanza ndani ya miaka 35 amefanya kazi ya hoteli kushuhudia kisa kama hicho.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment