WAPALESTINA 6 WAUAWA GAZA.

Wapalestina sita wameuawa katika mashambulizi ya mabomu yaliyo fanywa na Israel katika eneo la Gaza katika siku inayo hesabika kuwa ni ya mashambulizi makubwa tangu Israel iishambulie Palestina takribani wiki tatu zilizo pita.

Uchunguzi wa JICHOPEMBUZI umebaini kuwa watu wa familia saba wameuawa katika mpaka baina ya Israel na Palestina uliozingirwa.

Barabara zinaonekana kuwa tupu na moshi mweusi unaonekana kutoka katika eneo la Gaza huku mitambo ya umeme ikiwa imezimwa baada ya matanki ya mafuta kupigwa .

mmoja wa waliopoteza ndugu katika shambulio la gaza

Wanajeshi 10 wa Israel wameuawa siku ya jumatatu wakiwemo wapiganaji watano wa Hamas walioingia Israel kupitia maandaki ya chini kwa chini

Israel inasema imegundua mahandaki Ishirini na mbili ya chini kwa chini eneo la mpakani kuingia Israel yanayo unganisha mtandao mpana wa maandaki hayo.

maafisa wa Afya katika utawala wa palestina wanasema kuwa watu 60 wameuawa Israel inasema imeshambulia maeneo sitini yakiwemo makao yasio na mtu ya kiongozi wa kundi la Hamas Ismael Haniya na vituo vya Redio na runinga vya Hamas

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa nchi yake ni lazima ijiandae na operasheni ya muda mrefu katika ukanda wa Gaza.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Post a Comment